Habari za Punde

Maadhimisho Siku ya Vyama vya Ushirika Zanzibar.

Na.Mwashungi  Tahir  Maelezo      2-7-2021.

WAZIRI wa Nchi Afisi ya Rais Kazi,Uchumi na Uwekezaji Mudrik Ramadhani  Soraga  ametoa taarifa rasmi kila ifikapo tarehe 3 siku yaJumamosi  ya Mwanzo ya Mwezi wa Julai ya kila mwaka, ni Siku ya Ushirika Duniani.

Akitoa tamko  ndani ya vyombo vya habari amesema Maadhimisho  yatafanyika  katika Ukumbi  wa  Sheikh Idriss Abdul Wakil  Kikwajuni  Zanzibar  siku  iliyoteuliwa  na Shirikisho la  vyama  vya  Ushirika  Duniani (International Cooperative Allience) mwaka  1923,  na ilitangazwa rasmi na Mkutano Mkuu  wa Umoja wa  Mataifa tarehe16 Disemba Mwaka 1992,ambapo wanaushirika huadhimisha.

Amesema  madhumuni makuu  ya kuadhimisha ni  kutoa fursa  ya kuhamasishana na kupeana elimu miongoni  mwa  wanachama  juu  ya  dhana  na  umuhimu  wa  vyama  vya  ushirika  kwa maendeleo yao  kiuchumi  na kijamii.

Pia kuimarisha  ubia  na  mashirikiano  miongoni  mwa  Mashirikisho  ya Vyama  vya Ushirika kati ya nchi  mbalimbali , kwenye  shirikisho  la  Ushirika  la  Kimataifa  (International Cooperative  Allience  (ICA).

Vile vile  kuwapa fursa  wanaushirika  katika nchi zao kutathmini mafanikio na kuendeleza changamoto pamoja na  kuandaa  mikakati ya  kuendeleza vyamahivyo  katika nchi zao.

Amesema  Serikali  ya Mapinduzi  Zanzibar itaendelea kuyatekeleza maelekezo  mbali  mbali yanayotolewa na Jamhuri ya Kimataifa  ikiwemo pendekezo  la Shirika la Kazi Duniani (ILO  Recommendation  193) juu ya kuendeleza  na  kusimamia  vyama  hivyo.

Aidha Zanzibar  inaungana na wanaushirika  walioko Mataifa  mengine  duniani kuadhimisha  kwa misingi ya kutathmini  mchango wa vyama vya ushirika,  katika  kutatua  matatizo  ya msingi ya  kiuchumi  na kijamii  ya  wanachama  kwa  misingi  Uhiari  na kidemokrasia.

Amesema kuwapa  fursa  wanaushirika  kupima  jinsi  vyama  vyao  vinavyoendeshwa  kwa  kuzingatia  misingi  na kanuni  za Kimataifa,  Uzingatiaji  wa  Haki  za  Binaadamu,  Usawa  miongoni mwa  wanachama na  Utawala  Bora,kutafakari  kwa  kiasi  gani vyama  vinafuata  miongozo  ya  Sera  ya  Maendeleo ya  Ushirika  ya  mwaka  2014,Sheria ya vyama vya Ushirika ya (2018) na kanuni  zake.

Hata hivyo amesema kushajihisha Mshikamano na Demokrasia katika  vyama  , kuweka  mikakati  ili  vichangie  kufikia  malengo  ya  Dira  ya  Maendeleo  Zanzibar  ya mwaka  2020-2050 .  malengo  ya  Maendeleo  endelevu  (SDGs)   katika  kuondosha  njaa,  kuimarisha viwanda  vya  kiushirika, ubunifu,kushiriki  katika  uchumi  wa bluu  na kutekeleza  ajenda ya Afrika 2063.

Ujumbe wa mwaka huu  2021 ni “ Kwa  pamoja  Tujenge  Ushirika” Maudhui ya ujumbe huo ni kushajihisha sekta  zote  katika  jamii,  kutekeleza   juhudi  za  makusudi  ili  kuhakikisha kuwa  vyama  vinatatua  mahitaji  ya  wanachama  wao  pia  vinatoa  ajira  kwa  makundi  yote  yakiwemo  vijana,  wanawake  na  watu  wenye  ulemavu  na  wazee.

“Natoa wito kwa  wananchi  tujiunge au tuanzishe vyama vya ushirika katika maeneo tunayoishi ili kwa pamoja tushiriki  hatika  harakati  za  kuichumi  kwa maslahi  yetu  na  kuijenga  nchi  yetu”,alisema  Waziri  Mudrik.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.