Habari za Punde

Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Atembelea Chuo cha Kyela Polytechnic College.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akisalimiana na  viongozi wakati alipowasili kwenye viwanja vya Chuo cha Kyela  Polytechnic College  kutembelea Chuo hicho, Agosti  2, 2021. Kutoka kulia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera na  Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wanachuo wanaoseomea taaluma ya ususi wakati alipotembelea Chuo cha Kyela Polytechnic College Agosti 2, 2021. Wa tatu kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya  Waziri Mkuu Sera, Bunge,  Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa na wanachuo wa Chuo cha   Kyela Polytechnic College College wakati alipotembelea Chuo hicho, Agosti 2, 2021.  Kulia kwa  Waziri Mkuu ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama shati la kitenge lililoshonwa na  Wanachuo wa Chuo cha Kyela Polytechnic College wakati alipotembelea Chuo hicho

Moja kati ya majengo ya  Chuo cha Kyela Polytechnic College ambacho Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikitembelea, Agosti 2, 2021.

(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.