Habari za Punde

Balozi Mahmoud Kombo Akutana na Kamishna wa Uhamiaji Tanzania Dkt.Makakala Wajadili Changamoto za Uhamiaji.

Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo katika picha ya pamoja na Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Tanzania, Dkt. Anna Makakala baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi Ndogo za Uhamiaji Jijini Dar es Salaam 

Na Mwandishi wetu,                                                                                                                       

Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo amekutana kwa mazungumzo na Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Tanzania, Dkt. Anna Makakala katika Ofisi Ndogo za Uhamiaji Jijini Dar es Salaam. 

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao walijadilia masuala mbalimbali yanayowahusu Watanzania wanaoishi nchini Italia, Ugiriki na maeneo mengine ya uwakilishi yanayoratibiwa na Ubalozi wa Tanzania uliopo Rome.  

Masuala mengine yaliyogusiwa katika mazungumzo yao ni changamoto mbalimbali za WanaDiaspora wanazozikabili nchini Italia na kwingineko kuhusu masuala ya Uhamiaji. 

Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Tanzania, Dkt. Alimuahidi Balozi Kombo kufanikisha utatuzi wa changamoto zote hizo kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na ofisi za Balozi za Tanzania ulimwenguni kote ikiwemo Ubalozi wa Tanzania nchini Italia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.