Habari za Punde

Mhe Othman: Serikali imeazimia kutokomeza Polio na Surua kupitia chanjo


                                      

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman amesema kwamba serikali kupitia Wizara ya Afya imeaamua kufanya kampeni ya Chanjo ya Polio na Surua pamoja na matone ya Vatamin A ili kutokomeza maradhi hayo Zanzibar.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko Masingini Wilaya ya Magharib A Unguja alipozungumza katika Uzinduzi wa Chanjo ya  Surua , Polio na utoaji wa matone ya Vatamin A kwa watoto kuzuia na kudhibiti mripuko wa maradhi hayo.

Amesema kwamba hatua hiyo ya serikali ya kuandesha kampeni ya chanjo hizo ni baada ya kuwepo  mripuko wa maradhi hayo kuanzia Januari na mwezi Machi mwaka huu  ambapo jumla ya wagonjwa 17,500 wameripotiwa katika visiwa vya Unguja na Pemba .

Aidha Mhe. Othman amesema kwamba takwimu za hivi karibuni  zinaonesha kwamba  kwa kipindi cha  Mwezi Julai hadi  Novemba mwaka huu wa 2022 zaidi ya watoto 1,742 wenye umri chini ya miaka 15 wameugua suara na wanane kati ya hao walifariki dunia.

Hivyo mhe. Othman amewataka wazazi na walezi kuhakikisha kwamba wanaotoa ushirikiano wa kutosha kwa kuwapeleka watoto wote wanaopaswa kuchanjwa na kupatiwa matone ya Viaman A wanapatiwa ili kutokomeza maradhi hayo yanayoweza kusababisha upofu, kupooza na hata vifo.

Mhe. Othman amesema kwamba lengo la kampeni hiyo Kitaifa  ni katika jitihada za serikali kuhakikisha inazuia  uingiaji wa Ugonjwa wa Plio  hapa Zanzibar kulingana na mripuko wa maradhi hayo uliotolkea katika nchi jirani za Msumbiji  na Malawi.

Hivyo amesema kwamba wataalamu wa wizara ya Afya watahakikisha kupita nyumba kwa nyumba katika kampeni hiyo ili kuwachanja na kuwapatia matoni ya vitamin A watoto wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 350,000 katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Amesema kwamba serikali inafanya hivyo kwa kuzingatia kwamba kinga ni bora kuliko tiba na kwamba jitihada hizo zitasaidia kuudhibiti ugonjwa huo na kuutokomeza kabisa katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Aidha Mhe. Othma ameutaka uongozi wa wizara ya afaya kuongeza juhudi ya kutoa elimu ya Afya na uhamasishaji kwa jamii kuhusu umuhimu wa chanjo hizo kwa kuwa wapo baadhi ya wananchi wanaendelea kuwa na dhana  mbaya kuhusu chanjo hizo kwa watoto.

Aliitaka jamii kuthamini kwa vitendo msaada wa chanjo hiyo uliotolewa na Mahrikia  ya Kimataifa ili kusaidia kuendesha kampeni hiyo kwa mafanikio lengo kuu likiwa kulinda afya za watoto wote wa Zanzibar.

Naye Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazuri suala la utoaji wa chanjo mbali mbali liliyumba mnamo mwaka 2020 baada ya kuzuka maradhi ya Kovidi 19 na kwamba baada ya kudhibitiwa ugonjwa huo nguvu kubwa inaelekezwa katika chanzo za surua, Polio na utoaji wa matoni ya Vitamin A.

Amewataka wazanzibari wote wahamasiki na kuitikia wito wa wizara hiyo katika kuhakikisha watoto wote wanaostahiki kuchanjwa nchi kutote wanapatiwa chanjo hizo kwa juhudi za pamoja.

Kwa upande wake Mtalamu wa Chanjo kutoksa Shirika la Afya Duniani (who) Dk. Wilium Mwenge amesema kwamba Mashirika na wadau mbali mbali wa Afya Duniani , wanaunga mkono juhudi za serikali za na kwamba kwa pamoja wataendelea kutoa ushirikiano katika jitihada za kutokomeza ugonjwa huo.

Chanjo hizo za surua, polio pamoja na utoaji wa matoni yas Vitamin A imegharamiwa kwa Pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto (UNISEF), Sherika la Afya Duniani ( WHO) na shirika la GAVI ambapo shilingi milioni mia nane na sabiini na sita zimetolewa kugharamia chanjo hiyo .

 

 

Mwisho.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Kupitia Kitengo cha Habari leo tarehe 18.11.202.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.