Habari za Punde

Dk.Hussein Amewapongeza Wasanii kwa Kazi Kubwa Wanayoifanya Katika Kuburudisha na Kuelimisha Jamii

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, akizungumza na Msanii wa Kizazi Kipya (Bongo Fleva) Mbwana Yussuf Kilungi.(Mboso) alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewapongeza wasanii wa Wasafi, kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuburudisha na kuihamasisha jamii.

Dk. Mwinyi alitoa pongezi hizo Ikulu, Zanzibar alipozungumza na msanii Mbwana Yussufu maarufu Mbosso aliyefika hapo kwa mazungumzo.

Rais Mwinyi alisema wasanii ni kiungo chenye kufikisha ujumbe haraka kwa hadhira kutokana na mvuto mkubwa kwa jamii.

Aliwashukuru wasanii hao kwa utayari wao wanaoutoa nata kwenye sherehe za chama na Serikali kwa kazi kubwa ya buirudani jamii.

Naye, Msanii huyo aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mchango mkubwa inayowapa wasanii Tanzania.

Aliiahidi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kushirikiana nayo hasa kwenye masuala ya kijamii na kuwaeleza muda wote yupo tayari kulitumika taifa.

Alimueleza Dk. Mwinyi ujiuo wake kwa Zanzibar mbali na kufanyakazi kwa mashabiki wake lakini kupata baraka kwa viongozi wa Serikali na kumueleza Raisi kwamba yupo tayari kuchangia kwenye sekta ya maendeleo wakati wote.

Aidha, Mbosso alitumia fursa hiyo kumueleza Mke wa Rais wa Zanzibar ambae pia ni Mwenyekiti wa taasisi ya Maisha bora Foundation, Mama Maryam Mwinyi, kwamba yupo tayari kushirikiana na taasisi hiyo katika harakati za kuitumikia jamii kwa maendeleo.

Alisema Zanzibar ana mashabiki wengi wa muziki wake na kueleza ameamua kuufungua mwaka kivyengine Zanzibar na kuwaahidi mashabiki wake hushuhudia makubwa kwa aliyowatayarishia.

Akiwasilisha salamu za Mkurugenzi wa Wasafi Media, Abul Naseeb maarufu Diamond Platinum mbele ya Rais Mwinyi, Mkuu wa Idara ya Habari ya Wasafi media, Stancer Lameck alimueleza Dk. Mwinyi kwamba daima Wasafi wanaungamkono juhudi anazozifanya za kuifungua nchi kimaendeleo.

Alisema Diamond anaishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kuwafungulia milango ya fursa Wasafi na kuahidi watakua mabalozi wazuri wa kuitangaza Zanzibar kimataifa kupitia utalii.

Mbosso alianza muziki tokea akiwa na kundi la Yamoto wakati huo akitambulika kwa jina la Maramboso mnamo miaka 2013 kabla ya kusambaratika kwa kundi hilo kwenye miaka ya 2015 na baadae mwaka 2018 alifunga mkataba na kampuni ya WCB ya Wasafi ambako aliendeleza safari ya muziki wake.

Miaka miwili iliyopita nyota huyo wa muziki wa solo, bongo flava, mtunzi wa nyimbo na mpiga gitaa, Mosso alifanikiwa kupata mashabiki wengi zaidi kwenye kurasa zake za mitandao kwa wakati huo alifanikiwa kutimiza zaidi ya mashabiki milioni moja kwenye mtandao wake wa “yutube” .

Mwaka 2021 alifaikiwa kuiteka hadhira ya mashabiki wake kwa wimbo wake wa “Maana ya Mapenzi” (Definition of Love) aliyowashirikisha wasanii nguli wa bongo fleva akiwemo bosi wake, Diamond Platinum,  kundi la Njenje, Msanii maarufu kutoka Nigeria, Mr. Flavaur, Rayvanny, Liya, Daraaasa, Baba Levo na Diana.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.