Habari za Punde

Timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Yaibuka kidedea yaichapa Mahkama 3-2



 

Timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar imetwaa ubingwa katika mchezo wa kirafiki wa kuadhimisha siku ya sheria Zanzibar  baada ya kupata ushindi wa goli 3-2 dhidi ya timu ya Mahkama.

 

Mchezo huo uliopigwa katika dimba la Mao Zendong watunga sheria hao wa Baraza la Wawakilishi waliovalia jezi za kijani waliweza kuonesha soka safi na kuwafanya wapinzani wao kuruhusu magoli matatu ya papo kwa papo ambayo yalisimama hadi kumalizika kipindi cha kwanza.

 

Timu ya Mahkama walikianza kwa kasi kipindi cha pili na kufanikiwa kurudisha magoli mawili ambapo hadi mwamuzi wa kati anapuuliza kifirimbi cha kumaliza mchezo huo timu ya BLW walikuWa mbele kwa goli 3 – 2.

 

Ushindi huo umeendeleza mwendo mzuri wa timu ya watunga sheria hao kwa kucheza michezo ya mashindano  mbali mbali bila ya kupoteza.

 

Viongozi wa timu zote mbili za baraza la wawakilishi na mahkama wakauelezea mchezo huo pamoja na mipango yao katika kuzinoa timu zao  ili ziweze kuwa  bora zaidi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.