Habari za Punde

Wananchi wa Kijiji cha Kiyongwe Kupatiwa Ufumbuzi Changamoto Zinazowakabili

 SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeahidi kwamba itashughulikia Changamoto za wakaazi wa Kijiji cha Bumbwini Kiyongwe za ukosefu baadhi ya huduma muhimu za kijamii zinazowakabili ili kuleta ustawi bora wa maendeleo ya Kijamii.

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Cahama cha ACT- Wazalendo Zanzibar, ameeleza hayo huko Bumbwini kiyongwe Kaskazni B Unguja akiwa katika mfululizo wa ziara za kuwakagua  na kuwafariji wangonjwa na wananchi waliopatwa na misiba  katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema kwamba serikali imepokea kutoka kwa wananchi na kuona kuwepo kero kubwa ya ukosefu wa usafari wa barabara  jambo linalochangia kodhoofisha shughuli za kimaendeleo kwa wananchi wanaoishi kwenye kijiji hicho.

 Mhe. Othman amesema kwamba kero kubwa ya barabara, iliyopo inayochangia wahudumu wa afya na waalimu kutofika na kurudi kwa wakati katika vituo vyao vya kazi ndani ya kijiji hicho na kwamba suala hilo kero ambayo serikali italishughulikia na kulipatia ufumbuzi.

Kwa upande mwengine Mhe. Othman aliwaleza Viongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo katika ngazi ya wilaya na Mikoa kuiga mfano wa wenzao wa mjini kuanzisha mifuko ya faraja itakayotumika kusaidia kutatua changamoto mbali mbali walizonazo wananchi kwenye maeneo yao.

Aidha amewaka viongozi hao pia kuendeleza ziara  katika majimbo yao ili kuonana na kupokea changamoto mbali mbali zilizomo kwenye maeneo tofauti na kwamba kufanya hivyo ndio wajibu muhimu wa kiongozi kuwatumikia wananchi.

Mapema wakaazi wa Kijiji cha Kiyongwe walimueleza Mhe. Othman kwamba Kijiji hicho hakina barabara kwa muda mrefu sasa jambo linalochangia wananchi kupata shida ya kuingia na kutoka  katika kutekeleza shughuli zao za kimaendeleo za kila siku huku wahudumu wa afya na walimu wa skuli hiyo ikidhoofisha utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha wananchi hao walimueleza Mhe. Makamu kwamba kero kubwa ya barabara iliyopo katika kijiji hicho inachangia walimu pamoja na wahudumu wa Kituo cha Afya cha Kijiji cha Kiyongwe Kidogo kushindwa kufika kazini kwa wakati ili kuwahudumia wananchi kama inavyohitajika.

Wamesema kwemba wafanyakazi hao wanalazimika kukodi boda  boda kila siku ili kuweza kuingia na kutoka kazini ama kutembea masafa marefu kwa miguu jambo ambalo linachangia kupunguza ufanisi wa shughuli za utekelezaji wa  majukumu ya wafanyakazi hao kila siku.

Mhe. Othman katika ziara hiyo alitembelea katika Majimbo Bumbwini, Donge, Tumbatu,   Nungwi , Mkwajuni, Kiwengwa , Kijini , Chaani pamoja na Mahonda kuwakagua wagonjwa na watu waliofikwa na msiba ikiwa ni mfululizo wa kuendeleza ziara zilizokuwa zikifanywa na mtangulizi wake marehem Maaalim Seif Sharifu Hamad na kwamba ziara hiyo kesho itaendelea katika Mkoa wa Kusini Unguja.

MWISHO

Imetolewa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 27.03.2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.