Habari za Punde

Alhajj Dk.Hussein Mwinyi Ameitaka Jamii kwa Kila Mwenye Uwezo Kuendelea Kuwasaidia Wenye Uhitaji

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Watoto wenye ulemavu wa ngozi akiwa amembeba Mtoto Atra Suleiman, baada ya kumalizika kwa hafla ya kukabidhi sadaka ya vyakula kwa Wananchi wa Makundi Maalum wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, iliyofanyika katika viwanja vya Mapinduzi Square Michezani Muembekisinge Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar leo 14-4-2023

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameitaka jamii kwa kila mwenye uwezo kuendelea kuwasaidia wenye uhitaji ili kupata fadhila za mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Al- hajj Dk. Mwinyi aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi walio kwenye makundi maalumu wakiwemo wazee, wajane, watoto yatima na wenye ulemavu huko viwanja wa Mapinduzi Square, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Alisema Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni mwezi wa neema na inampendeza Mola, watu wote kuishi kwa upendo, ushirikiano na kusaidiana hasa kwa jamii zenye uhitaji zisaidiwe kwa kadri ya uwezo watu waliojaaliwa nao.

Alisema msaada wa vyakula uliotolewa na taasisi ya Maendeleo ya “Zanzibar International Development Organization” umekuja wakati jamii unauhitaji, hivyo, Rais Dk. Mwinyi aliendelea kutoa wito kwa wadau wengine na wananchi wenye uwezo kuendeleza moyo wa kuwasaidia wengine wenye uhitaji ili kujenga jamii yenye kumpendezesha Mwenyezi Mungu.

“Chakula hiki kuwapa watu wasiokua na uwezo, Mwenyezi Mungu awalipe pepo ndegu zetu wafadhili hawa” Dk. Mwinyi aliwaombea Kheri wafadhili waliotoa msaada huo wa vyakula kwa makundi maalum.

Aidha, Rais Mwinyi, aliishukuru taasisi ya maendeleo ya “Zanzibar International Development Organization” ambao walijitolea kutoa msaada huo wa vyakula na mahitaji mengine kwa jamii hio.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, mmoja wa wanufaika wa sadaka hiyo, Jamila Boraafya (Mwenye ulemavu wa kuona) alimshururu Rais Dk. Mwinyi kwa jitihada anayoichukua kuwafikia wananchi wake wa makundi yote.

Alisema uongozi wake umekua mfano wa kuigwa wa viongozi wengine wa ngazi zote katika kuwahudumia wanaowangoza.

“Tunakushukuru sana Mhe. Rais Dk. Mwinyi, juhudi zako tunaziona na upendo wako kwetu wananchi wako, hakika wewe ni kiongozi wa mfano na Mwenyezi Mungu ataendelea kukulipa mema kwa kututumikia, unafika hadi mataifa ya nje kwaajili ya kutuhangaikia sisi wananchi wako, ahsate sana na Mola azidi kukulipa kheri” alishukuru Jamila.

Zoezi kama hilo la ugawaji wa sadaka ya iftari kwa mwezi huu mtukufu Ramadhan, Rais Dk. Mwinyi pia alilifanya kwa Wilaya nne za Pemba kwa mikoa yote ya Kusini na Kaskazini wakati wa ziara yake ya siku mbili kisiwani himo, iliyomalizika hivi karibuni.

IDARA YAMAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.