Habari za Punde

Kampuni ya Edmark kusaidia vijana kupata ajira

Meya wa Jiji la Zanzibar, Mhe, Mahmoud Mohamed Mussa akitoa nasaha kwa wanachama wa Kampuni ya Edmark katika sherehe ya kutimiza miaka mitatu tangu kufunguliwa tawi la Zanzibar  huko Ofisini kwao Mombasa Wilaya ya Magharibi ‘B’
Meneja Msaidizi wa Kampuni ya Edmark  Ms Maylyn akitoa maelezo ya bidhaa mpya zinazotarajiwa kufika mwishoni mwa mwaka huu, katika sherehe ya kutimiza miaka mitatu tangu kufunguliwa tawi la Zanzibar huko Ofisini kwao Mombasa Wilaya ya Magharibi ‘B’
Baadhi ya wanachama na ambao sio wanachama wakisikiliza mafunzo ya matibabu ya dawa zinazotengenezwa na Kampuni ya Edmark yaliyotolewa na Dr Salma Chande kutoka Tanzania Bara  (hayupo pichani)  katika sherehe ya kutimiza miaka mitatu tangu kufunguliwa tawi la Zanzibar huko Ofisini kwao Mombasa Wilaya ya Magharibi ‘B’

Na Khadija Khamis, Maelezo, 30/07/2023 .

Meya wa Jiji la Zanzibar,Mhe. Mahmoud Mohamed Mussa amesema Kampuni  ya Edmark itawasaidia vijana kujipatia ajira kuepukana na kujiingiza katika vitendo viovu vya kutumia madawa ya kulevya.

Hayo ameyasema huko Mombasa katika Kampuni ya Edmark wakati wa sherehe ya kutimiza miaka mitatu tangu kufungua kwa Tawi lake  hapa Zanzibar  huko Ofisini kwao Mombasa Wilaya ya Magharibi 'B'..

Amesema kwamba iwapo vijana watakidhi vigezo vyao wawasaidie kuwachukuwa ili kujipatia ajira na  kujiepusha  kukaa vijiweni ambako kunavishawishi vya aina  mbali mbali ikiwemo kujiingiza katika uraibu wa madawa ya kulevya .

Aidha alifahamisha kuwa serikali zote mbili ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hazikubaliani na mambo ya jinsia moja  aliwataka wazazi na walezi kuwaelimisha vijana wao ili wasijiingize katika mlolongo wa mambo hayo .

Meya Mahmoud akizungumzia suala zima la udhalilishaji na kuwataka akibaba kujitahidi kuwatunza akinamama na watoto ili kuwe naTaifa lililobora nchini .

“Tujitahidi kuwalinda na kuwasaidia watoto wetu kwani watoto tulionao ndio taifa letu la kesho ,” alisema  Meya Mohmoud .

Alieleza kuwa kwa taarifa alizopokea kutoka Ofisi ya Mufti talaka zimekuwa nyingi jambo ambalo linachangia mmon’gonyoko wa maadili hivyo aliitaka jamii kujitahidi kuzidumisha ndoa zao ili mambo yawe sawia.

Vile vile aliiyomba kampuni hiyo kuyaendeleza yale mazuri ambayo wanania ya kuyafanya ili iwe chachu ya kuwasaidia wazanzibar na watanzania kwa ujumla na Serikali ipo pamoja nao ili kuhakikisha kunaondokana na  changamoto zilizopo na  kuijenga Zanzibar yenye umoja mshikamano kwa maslahi ya vizazi vijavyo.

Nae Meneja Msaidizi wa Kampuni ya Edmark  Ms Maylyn alisema hivi karibuni watazindua bidhaa zao mpya ambazo zitawasaidia watu wenye changamoto ya macho.

Aidha alisema bidhaa yao ya splina liquid ya kusawazisha mmengenyo wa chakula katika mtumbo mpana wanatarajia kuzileta za vidonge ili kurahisisha uchukuaji wa wateja wanaosafiri nje ya nchi .

Kwa upande wa Dr Salma Chande kutoka Tanzania Bara akitoa  elimu kwa wanachama hao alisema kuwa saratani ya utumbo mpana ni gonjwa namba moja kwa kuua watu katika karne ya 21.

Aliiyomba jamii kuacha ulaji wa chakula cha uwanga katika nyakati za usiku kwani  ni hatari kwa afya zao aliwataka kutumia   matunda na mboga mboga kwani wakati wa kulala hakuna mmengenyo wa vyakula ila vyakula vyote hugeuzwa kuwa  mafuta .

Aidha alisema dalili kuu ya magonjwa sugu huanza tumboni bacteria humengenya na kuzalisha sumu za aina tatu na kiwango kikubwa cha tendikali  kinasababisha uzee wa mapema na unene wa kupitiliza .


 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.