Habari za Punde

Mafunzo Kwa Mafundi Mchundo wa Majokofu na Viyoyozi

Mkufunzi kutoka Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) cha Bagamoyo Mkoa wa Pwani, Mhandisi Goodluck Rulagora akitoa mafunzo kwa vitendo kwa baadhi ya mafundi mchundo na viyoyozi kutoka Jijini Dar es Salaam ambao wanashiriki warsha ya mafunzo kuhusu utekelezaji wa Itifaki ya Montreal inayohusu Kemikali zinazomong'onyoa Tabaka la Ozoni, jijini Dar es Salaam 
Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Kemilembe Mutasa (katikati) akizungumza na baadhi ya mafundi mchundo wa viyoyozi na majokofu wa jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kuhusu utekelezaji wa Itifaki ya Montreal inayohusu Kemikali zinazomong'onyoa Tabaka la Ozoni, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Serikali imetoa rai kwa mafundi mchundo wa viyoyozi na majokofu kuzingatia matumizi salama ya kemikali wakati wa kuhudumia vifaa hivyo ili kuepuka kusambaa angani kwa kemikali au gesi hizo na kusababisha uharibifu wa tabaka la ozoni au ongezeko la joto duniani.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira 

Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Kamilembe Mutasa wakati 

akifungua mafunzo kuhusu utekelezaji wa Itifaki ya Montreal 

inayohusu Kemikali zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni leo 

Mei 06, 2024 jijini Dar es Salaam.

Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa 

mafundi hao kuhusu matakwa ya itifaki hiyo ambapo 

wanasayansi walivumbua kemikali hizo mwanzoni mwa miaka 

ya 1970 ambazo hujipenyeza angani na kumong’onyoa tabaka 

la hewa ya ozoni kwa kuruhusu mionzi au miale ya jua kufika 

katika uso wa dunia na kusababisha madhara kwa afya ya 

binadamu na mazingira.

Bi. Kemilembe ametaja madhara hayo kuwa ni magonjwa ya 

saratani ya ngozi, uharibifu wa macho unaosababisha upofu 

na athari kwa ukuaji wa mimea na viumbe hai wengine.

Amesema kemikali zinazoharibu tabaka hilo zinatumika 

katika majokofu na viyoyozi, vifaa vya kuzima moto, usafishaji chuma, utengenezaji magodoro, ufukizaji wa udongo katika vitalu vya tumbaku na kilimo cha maua na hifadhi ya nafaka katika maghala.

Kutokana na changamoto hiyo, Bi. Kemielembe amesema 

juhudi zimeendelea kufanyika tangu mwaka 1985 baina ya 

Serikali kitaifa na kimataifa kukubaliana kuanzisha Mkataba 

wa Vienna na Hifadhi ya Tabaka la Ozoni na hatimaye Itifaki 

ya Montreal kuhusu udhibiti wa kemikali zinazomong’onyoa 

Tabaka la Ozoni ambapo shabaha yake kuu ni kusitisha 

utengenezaji na utumiaji wa kemikali zinazomong’onyoa 

Tabaka la Ozoni.


Ameongeza kuwa Itifaki ya Montreal imekuwa ikifanyiwa 

marekebisho mbalimbali kutokana na tafiti zinazoainisha 

kemikali mbalimbali zinazomong’onyoa tabaka la ozoni au 

kuwa na athari zingine za kimazingira kama kusababisha 

ongezeko la joto duniani.


Hivyo, mafunzo hayo yanayohusu njia bora za kuhudumia 

vifaa ikiwemo majokofu na viyoyozi pasipo kuathiri mazingira 

yanatolewa na Mtaalamu wa Kimataifa wa viyoyozi na 

majokofu kutoka Shirika la Umoja wa Kimataifa la Mazingira 

(UNEP) Bw. Freeborn Taruvinga kwa kushirikiana na 

wakufunzi kutoka Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi 

(FETA), Bagamoyo Mhandisi Goodluck Rulagora pamoja na 

Bw. Said Mziwanda koka kutoka Chuo cha Mafunzo ya Elimu 

ya Ufundi Stadi (VETA) Chang’ombe, jijini Dar es Salaam 

chini ya shughuli wezeshi ya kujenga uwezo wa kitaasisi katika kutekeleza Itifaki ya Montreal inayotekelezwa na kuratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.