Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe. Leontine Nzeyimana katika picha ya pamoja alipowasili kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akihutubia wageni waalikwa kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato amepoingeza Jamhuri ya Burundi kwa kuendelea kulinda na kudumisha amani na usalama nchini humo.
Naibu Waziri Byabato amasema hayo alipokuwa akihutubia Jumuiya ya Wadiplomasia na wageni wengine waalikwa kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Vilevile alibainisha kuwa katika kipindi hicho cha miaka 62 dunia imeshuhudi Taifa hilo likipiga hatua muhimu ya maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo siasa na uchumi.
“Hakika mtakubaliana nami kuwa katika kipindi cha miaka
62, Burundi imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika nyanja
za kisiasa na kiuchumi. Mathalani, kisiasa tangu kusainiwa
kwa Mkataba wa Amani hapa jijini Dar es Salaam mwaka
2006, Burundi imeweza kudumisha amani na usalama
nchini kote pamoja na kukuza demokrasia na utawala
bora” Alieleza Naibu Waziri Byabato
Mbali na hayo Waziri Byabato aliongeza kuwa Tanzania na
Burundi zimeendelea kuwa na ushirikiano wa karibu wakati
wote, ukichagizwa na mkaba uliosaniwa mwaka 1975 wa
uanzishaji wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ambao ulifungua
ushirikiano katika sekta mbalimbali za kimkakati ikiwemo
elimu, afya, kilimo, biashara na uwekezaji, utalii,nishati,
usafirishaji, ulinzi na usalama na masuala ya uhamiaji.
Kwa upande wake Balozi wa Burundi nchini Tanzania
Mhe. Leontine Nzeyimana alieleza kuwa katika kipindi cha
miaka 62 ya uhuru, Taifa hilo linajivunia kuendelea
kudumisha uhusiano mzuri wa kidiplomasia na Mataifa
mbalimbali duniani na nchi jirani katika Kanda ya Afrika
Mashariki.
Balozi Nzeyimana aliendelea kubainisha kuwa katika nyanja
ya uchumi Burundi inaendelea kushirikiana na wadau
mbalimbali wa maendeleo ikiwemo Tanzania, ambapo mradi
wa SGR unatarajiwa kuliunganisha Taifa hilo na Bandari ya
Dar es Salaam hivyo kutoa mchango mkubwa katika
kurahishisha na kuongeza biashara na uwekezaji kati ya
Tanzania na Burundi.
Takwimu zinaonyesha kuwa biashara kati ya Tanzania na
Burundi inaendelea kukua ambapo ilifikia dola milioni 212.8
mwaka 2022/2023 kutoka dola 61.3 milioni mwaka
2017/2018. Huku takriban asilimia 95 ya mizigo ya Burundi
ikipitia Bandari ya Dar es Salaam.
Tanzania na Burundi zinashirikiana kwa karibu katika ngazi za
kikanda na kimataifa ikiwemo EAC, ICGRL, AU, UN, Jumuiya
ya Nchi zisizofungamana na Siasa za Upande wowote (NAM).
Aidha Naibu Waziri Byabato alisisitiza dhamira ya Serikali ya
Tanzania ya kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya
Burundi ili kuimarisha zaidi uhusiano kwa manufaa ya pande
zote mbili na watu wake. Vile vile, kuendelea kuwa mshirika
wa wakati wote na wa kuaminika wa Burundi kwenye masuala
ya kikanda na kimataifa.
No comments:
Post a Comment