Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA, Mhandisi Aron Joseph
ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kutoa kiasi hicho
cha fedha kwa wananchi waliyotoa ardhi yao kupisha
utekelezaji wa miradi ya maji.
"DUWASA, kwa niaba ya Wananchi wa maeneo ya Nzuguni,
Zuzu Nala, Nala Chihoni na Kibaigwa, inaishukuru Serikali ya
Awamu ya Sita na Wizara ya Maji kwa juhudi zao kubwa na
ufanisi katika kuhakikisha ulipaji wa fidia kwa wakati kwa
wananchi wetu," alisema Mhandisi Aron.
"Hatua hii ni muhimu sana kwa maeneo yaliyotekelezwa na
yanayoendelea na utekelezaji wa miradi ya maji ya kimkakati
katika Jiji la Dodoma na Kanda ya Kibaigwa, hii inaonesha
dhamira ya Serikali katika kulinda haki za wananchi wakati
wa kutekeleza miradi ya maendeleo." Amesma Mhandisi Aron.
Kwa upande wa wakazi wa Kibaigwa, Bi. Josephina Paulo
ameishukuru serikali kwa kuwasikiliza na kuwalipa fidia.
Ameiomba serikali kwa kuwaona wanyonge na kuwafikia
wengine ambao bado hawajalipwa wanasubiri
kulipwa.
Naye Bwa. Yohana Mwarabu ameshukuru serikali kwa
kumjali na kumlipa kwani sasa ataenda kujenga nyumba
nyingine ili aweze kuishi na familia yake kwani awali hakuwa
na matumaini lakini kwa sasa anaamani.
Fidia hiyo ni sehemu ya maandalizi ya ujenzi wa miradi
mbalimbali ya maji inayotekelezwa na Serikali kupitia
DUWASA iliyokusudiwa kuboresha upatikanaji wa majisafi na
huduma za usafi wa mazingira ka wakazi wa jiji la Dodoma na
maeneo mengine yanayohudumiwa na DUWASA.
No comments:
Post a Comment