Habari za Punde

uzinduzi wa Muongozo wa Kitaifa wa Stadi za Maisha Kwa Vijana walio nje ya Skuli Zanzibar

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Ndugu Fatma Hamad Rajab  amezitaka Taasisi na Wadau mbali mbali  wa Maendeleo ya Vijana kutoa Mafunzo ya muongozo wa Stadi za Maisha kwa Vijana ili kuweza kujitambua .

Ameyasema hayo wakati wa hafla ya  uzinduzi wa  Muongozo wa  Kitaifa wa  Stadi za Maisha Kwa Vijana walio nje ya Skuli Zanzibar Katika ukumbi wa Sheikh  Idrisa Abdul - Wakil  Kikwajuni.

Amesema Vijana wamekuwa wakikabiliwa na changamoto  mbali mbali katika jamii pamoja na familia,  jambo ambalo husababisha msongo wa mawazo na hupelekea kujiingiza  Katika Tabia hatarishi.

Aidha amesema muongozo huo unalenga kutatua changamoto mbali mbali ikiwemo Afya ya Uzazi, unyanyasaji wa kijinsia, madawa ya Kulevya matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano lishe na Ajira Kwa vijana.

Amefahamisha kuwa Stadi hizi huwafundisha Vijana namna ya kujiamini, Kudhibiti hisia, kutatua changamoto pamoja na kufanya Maamuzi sahihi.

"Suala la Stadi za Maisha ni ujuzi na fani muhimu za kuwawezesha Vijana kukabiliana na changamoto za Kila siku Kwa  kuweza kufanya Maamuzi sahihi na kuishi Kwa Amani na Furaha na watu wengine " amesema Katibu Fatma 

Amesema Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa  kushirikiana na Wadau mbali mbali  wa Maendeleo  walifanya mchakato  wa marekebisho ya  Mwaka 2019 ili kukidhi  mahitaji ya Sasa.

Nae Mkurugenzi wa  Idara ya Maendeleo ya Vijana Shaib ibarahim Mohamed  amesema lengo la  muongozo wa Stadi za Maisha Kwa Vijana ambao wapo nje ya Skuli ni kuzitaka Taasisi na Asasi za Kiraia  kutoa Mafunzo sahihi yanayoendana na mazingira, Utamaduni wa Zanzibar pamoja na Sheria za nchi.

Nae Muwakilishi wa Shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia Watoto UNICEF Laxmi Bhawan amesema kitini hicho kitakuwa ni chachu  ya kuleta matokeo chanya Katika Maisha ya vizazi vya Sasa na  vijavyo..

Amesema Mafunzo ya Stadi za maisha yatasaidia  kumbadilisha Kijana kiakili, kihisia, kiimani pamoja na kimuonekano jambo ambalo husaidia kuondokana na changamoto na kuwa na maamuzi sahihi.










No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.