
Na
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
YANGA,
inayokabiliwa na kibarua cha kutetea ubingwa wa klabu Afrika Mashariki na Kati
kupitia mashindano ya Kombe la Kagame,
itaanza kampeni zake Julai 14 mwaka huu kwa kuwavaa wawakilishi wa Burundi,
timu ya Atletico kwenye uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam.
Taarifa
hiyo ni kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki
na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye, katika mkutano na waandishi wa habari
uliofanyika jana kwenye ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Timu
11 zinatarajiwa kushiriki patashika hizo, zitakazoanza Julai 14 hadi 28 mwaka
huu, huku kila siku zikichezwa mechi
mbili, saa 8 mchana na saa 10 jioni, ambapo mbali na Yanga, Tanzania Bara
itawakilishwa pia na klabu za Simba na Azam.
Ratiba
ya mashindano hayo inaonesha kuwa, mechi ya kwanza siku ya ufunguzi ambayo
itachezwa saa 8:00 mchana, itazikutanisha timu za APR ya Rwanda na Wau Salaam
ya Sudan Kusini.
Katika
kundi A la michuano hiyo, kutakuwa na timu za Simba, URA ya Uganda, Vita Club
ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na Ports ya Djibouti, ambapo Azam FC,
Mafunzo ya Zanzibar na Tusker ya Kenya ziko katika kundi B.
Kundi
C linaundwa na timu za Yanga, APR ya Rwanda, Wau Salaam ya Sudan Kusini na
Atletico ya Burundi.
El
Merreikh ya Sudan, Red Sea ya Eritrea, Coffee ya Ethiopia na Elman ya Somalia
hazitashiriki katika mashindano ya mwaka huu ambayo yanafanyika Tanzania Bara
kwa mwaka wa tatu mfululizo kutokana na sababu mbalimbali.
Coffee
haitashiriki kwa vile ligi ya Ethiopia inaanza Julai 14 mwaka huu wakati El
Merreikh itakuwa na mechi ya michuano ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), kati
ya Julai 13 na 15.
Fedha
za zawadi kwa bingwa wa michuano hiyo hutolewa na Rais wa Rwanda Paul Kagame,
ambapo bingwa atazoa dola elfu 30,
makamu bingwa dola elfu 20 na mshindi wa tatu dola elfu kumi.
0 Comments