6/recent/ticker-posts

Unicef kuendelea kusaidia taaluma katika nyanja za afya , elimu na jamii

 Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Rafii Haji Makame (kulia) akitoa ufafanuzi wakati wa mazungumzo yake na Ujumbe wa UNICEF yaliyofanyika Ofisi ya Tume ya Utangazaji Kikwajuni
Ujumbe wa UNICEF ulipokuwa na mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo katika Ofisi ya Tume ya Utangazaji Kikwajuni jana.
(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

Khadija Khamis na Patima Mtumwa – Maelezo Zanzibar 25/09/2013.
 
Shirika  la  Umoja wa Mataifa  linaloshughulikia  Watoto UNICEF limeonyesha azma  ya  kuendelea kusaidia kutoa taaluma katika nyanja za Afya, Elimu na Jamii nchini.
 
Shirika  hilo kupitia Taasisi za Habari na Mawasiliano  limeahidi kusaidia katika  kuaandaa  vipindi  vya Radio na TV kwa lengo la kuelimisha jamii   mjini na vijijini.
 
Maafisa wa Shirika hilo wakiongozwa na Mkurugenzi wake Elephase Kamugushi  wameeleza hayo walipokutana  na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Rafii Haji  katika ukumbi wa Tume ya Utangazaji  Kikwajuni  mjini Zanzibar .
 
Kamugisha ametaka  vipindi hivyo vielekezwe katika kuelimisha matatizo yanayowakabili watoto ikiwemo ajira za watoto, watoto  wanaoishi katika mazingira magumu pamoja na  maradhi yanayowasumbua watoto ikiwemo cholera, malaria  na  utapia mlo.


Amesema UNICEF litasaidia upatikanaji wa nyenzo za kufanyia kazi na utaalamu ili kuviwezesha vipindi hivyo kuwa na mvuto kwa wasikilizaji.
 
 Kamugisha ameahidi kukutana na Wizara na Taasisi  zinazoshughulikia watoto Zanzibar ili kuhakikisha azma hiyo ya UNICEF inafanikiwa.
 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Rafii Haji  Makame alieleza  kufarijika na uamuzi huo wa UNICEF  ambao  umeleta  faraja hasa wakati huu ambapo Zanzibar inaandaa vipindi mbali mbali kwa ajili ya Sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi.
 
Alisema  Idara ya Habari Maelezo imeanzisha utaratibu wa kuonyesha vipindi vijijini kwa njia ya senema na kumekuwa na upungufu mkubwa wa vipindi, hivyo msaada wa UNICEF utasaidia kupatikana kwa vipindi vya uhakika.
 
 Mkurugenzi Rafii amelishukuru Shirika hilo kwa msaada wake huo na ameahidi kusimamia kikamilifu kuhakikisha vipindi vinavyowahusu watoto vinaandaliwa kwa wingi.


Post a Comment

0 Comments