
Shamuhuna Asema Amefanya Kazi Tokea Awamu ya Kwanza
Atahakikisha Maslahi ya Zanzibar Yanalindwa
Ataridhia Mabadiliko Yanayolinda Muungano
NAIBU Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari Utamaduni na Mchezo, Ali Juma Shamuhuna
amesema yeye ni kiongozi shupavu wa kisiasa anayekubali mabadiliko ambayo hayageuzi misingi ya kisiasa.
Alisema kwa vile amefanya kazi na awamu zote sita nchini, ataridhia mabadiliko yatakayolinda Muungano, yatakayoheshimu misingi ya CCM katika utawala, uchumi na maendeleo.
Aidha alieleza kuwa mabadiliko mengine ni yake yanayotetea usawa wa binaadamu, jinsia na kuheshimu katiba, sheria na kanuni za kuendesha nchi katika utawala bora.
Alifafanua kuwa, endapo atapewa ridhaa ataendeleza sera zilizopo na kubuni sera na mipango mipya itakayosaidia kuendeleza uchumi wa Zanzibar na ustawi wa wananchi wake, kwa kuhakikisha maisha yao yanaimarika siku hadi siku.
Alisema atahakikisha mafuta yatabakia kuwa si ya Muungano ingawa katika katiba ni Muungano lakini kimantiki ni ya Zanzibar, hivyo ataendeleza mazungumzo katika kutatulia hilo ili yaweze kusaidia kukuza uchumi wa visiwa hivi.
Akizungumzia msimamo wake juu ya kura ya maoni, alisema anaheshimu maamuzi ya Butiama na Chama chake, lakini alishauri suala hilo waachiwe wananchi waweze kuamua.
Shamuhuna aliijinadi kwamba anazo sifa za kuwa Rais wa Zanzibar na anafaa lakini wananchi na wapiga kura ndiyo wenye uwezo, haki na uhuru wa kumpima, kumchambua na hatimaye kuamua kama anafaa.
amesema yeye ni kiongozi shupavu wa kisiasa anayekubali mabadiliko ambayo hayageuzi misingi ya kisiasa.
Alisema kwa vile amefanya kazi na awamu zote sita nchini, ataridhia mabadiliko yatakayolinda Muungano, yatakayoheshimu misingi ya CCM katika utawala, uchumi na maendeleo.
Aidha alieleza kuwa mabadiliko mengine ni yake yanayotetea usawa wa binaadamu, jinsia na kuheshimu katiba, sheria na kanuni za kuendesha nchi katika utawala bora.
Alifafanua kuwa, endapo atapewa ridhaa ataendeleza sera zilizopo na kubuni sera na mipango mipya itakayosaidia kuendeleza uchumi wa Zanzibar na ustawi wa wananchi wake, kwa kuhakikisha maisha yao yanaimarika siku hadi siku.
Alisema atahakikisha mafuta yatabakia kuwa si ya Muungano ingawa katika katiba ni Muungano lakini kimantiki ni ya Zanzibar, hivyo ataendeleza mazungumzo katika kutatulia hilo ili yaweze kusaidia kukuza uchumi wa visiwa hivi.
Akizungumzia msimamo wake juu ya kura ya maoni, alisema anaheshimu maamuzi ya Butiama na Chama chake, lakini alishauri suala hilo waachiwe wananchi waweze kuamua.
Shamuhuna aliijinadi kwamba anazo sifa za kuwa Rais wa Zanzibar na anafaa lakini wananchi na wapiga kura ndiyo wenye uwezo, haki na uhuru wa kumpima, kumchambua na hatimaye kuamua kama anafaa.

Nitaendeleza umoja, amani, mshikamano wa Wazanzibari
Siasa za malumbano, chuki hazina nafasi
Atasimamia nidhamu, uwajibikaji serikalini
Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha jana aliungana na wagombea wengine sita wa nafasi ya Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi katia uchukuaji fomu za kuwania nafasi hiyo.
Alikabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Kamati Maalum, Itikadi na Uenezi, Zanzibar, Vuai Ali Vuai, Afisi kuu ya CCM, Kisiwandui.
Akizungumza na waandishi wa habari, alisema akichaguliwa atahakikisha amani, utulivu na umoja unaendelea kwa ajili ya kuendeleza maendeleo ya kiuchumi na kujenga Zanzibar yenye matumaini kwa wananchi wake.
Alieleza siasa za malumbano na za chuki hazina nafasi katika Zanzibar kwa sasa baada ya maridhiano yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambapo aliahidi kuiendeleza hali hiyo.
Alifahamisha kuwa, Zanzibar inahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja ya elimu ili kuwapatia taaluma iliyobora wananchi katika kukabiliana na soko la Afrika Mashariki na Kati, sambamba na kuimarisha kilimo hasa cha umwagiliaji na uvuvi .
Alisema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Karume imefanya kazi vizuri katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Unguja na Pemba, katika kusambaza miuondo mbinu ya barabara, maji, afya na elimu, ambapo matunda hayo atayaendeleza.
Hata hivyo, alisema atakakikisha anasimamia uwajibikaji na nidhamu katika sehemu za kazi kuanzia kwa Makatibu Wakuu, Wakurugenzi hadi kwa wananchi wa chini katika kufanya kazi kwa ufasini katika kuibadilisha Zanzibar.
Atasimamia nidhamu, uwajibikaji serikalini
Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha jana aliungana na wagombea wengine sita wa nafasi ya Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi katia uchukuaji fomu za kuwania nafasi hiyo.
Alikabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Kamati Maalum, Itikadi na Uenezi, Zanzibar, Vuai Ali Vuai, Afisi kuu ya CCM, Kisiwandui.
Akizungumza na waandishi wa habari, alisema akichaguliwa atahakikisha amani, utulivu na umoja unaendelea kwa ajili ya kuendeleza maendeleo ya kiuchumi na kujenga Zanzibar yenye matumaini kwa wananchi wake.
Alieleza siasa za malumbano na za chuki hazina nafasi katika Zanzibar kwa sasa baada ya maridhiano yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambapo aliahidi kuiendeleza hali hiyo.
Alifahamisha kuwa, Zanzibar inahitaji mabadiliko makubwa katika nyanja ya elimu ili kuwapatia taaluma iliyobora wananchi katika kukabiliana na soko la Afrika Mashariki na Kati, sambamba na kuimarisha kilimo hasa cha umwagiliaji na uvuvi .
Alisema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Karume imefanya kazi vizuri katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Unguja na Pemba, katika kusambaza miuondo mbinu ya barabara, maji, afya na elimu, ambapo matunda hayo atayaendeleza.
Hata hivyo, alisema atakakikisha anasimamia uwajibikaji na nidhamu katika sehemu za kazi kuanzia kwa Makatibu Wakuu, Wakurugenzi hadi kwa wananchi wa chini katika kufanya kazi kwa ufasini katika kuibadilisha Zanzibar.
No comments:
Post a Comment