
Bilal Aahidi Kuleta Maridhiano Kwa Wazanzibari
Asema Atasimamia Rasilimali Za Nchi
Aahidi Kuimarisha Elimu, Afya, Ajira Kwa Wote
WAZIRI Kiongozi Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Mohammed Gharib Bilal, amesema iwapo jina lake litapitishwa na baadae kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar, atahakikisha analeta maridhiano ya Wazanzibari wote.
Dk. Bilal alitoa kauli hiyo katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Ocean View jana, baada ya kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kuwa mgombea wa kiti hicho katika uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwezi wa Oktoba.
Alisema jambo lililofanywa na Rais Amani Abeid Karume anayemaliza muda wake na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad kufungua ukurasa mpya wa maelewano ni jema lakini linapaswa kwenda mbali zaidi ili kujenga umoja na maridhiano kwa wananchi wote wa visiwa hivi.
Alisema katika dunia hakuna mtu asiyependa maelewano, na kwamba kama atachaguliwa serikali yake haitakuwa na siasa za kulipa kisasi kwa kuwa yeye binafsi haoni kama amekosewa na yeyote.
Akizungumzia namna atakavyoleta ustawi wa kiuchumi kwa Zanzibar na wananchi wake, Dk. Bilal alisema atahakikisha rasilimali zote zilizomo nchini zinatumiwa kwa manufaa ya Wazanzibari wote.
Alisisitiza kuwa hatakuwa na muhali kwa yeyote katika suala la kuwajibika, na kuweka wazi kuwa kila atayepewa dhamana atalazimika kuitimiza mujibu wake.
Waziri Kiongozi huyo Mstaafu, alieleza kuwa pamoja na maendeleo yaliyofikiwa katika sekta za elimu na afya, ni lazima ziimarishwe.
WAZIRI Kiongozi Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Mohammed Gharib Bilal, amesema iwapo jina lake litapitishwa na baadae kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar, atahakikisha analeta maridhiano ya Wazanzibari wote.
Dk. Bilal alitoa kauli hiyo katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Ocean View jana, baada ya kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kuwa mgombea wa kiti hicho katika uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwezi wa Oktoba.
Alisema jambo lililofanywa na Rais Amani Abeid Karume anayemaliza muda wake na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad kufungua ukurasa mpya wa maelewano ni jema lakini linapaswa kwenda mbali zaidi ili kujenga umoja na maridhiano kwa wananchi wote wa visiwa hivi.
Alisema katika dunia hakuna mtu asiyependa maelewano, na kwamba kama atachaguliwa serikali yake haitakuwa na siasa za kulipa kisasi kwa kuwa yeye binafsi haoni kama amekosewa na yeyote.
Akizungumzia namna atakavyoleta ustawi wa kiuchumi kwa Zanzibar na wananchi wake, Dk. Bilal alisema atahakikisha rasilimali zote zilizomo nchini zinatumiwa kwa manufaa ya Wazanzibari wote.
Alisisitiza kuwa hatakuwa na muhali kwa yeyote katika suala la kuwajibika, na kuweka wazi kuwa kila atayepewa dhamana atalazimika kuitimiza mujibu wake.
Waziri Kiongozi huyo Mstaafu, alieleza kuwa pamoja na maendeleo yaliyofikiwa katika sekta za elimu na afya, ni lazima ziimarishwe.
Kinachonishangaza kidogo katika picha hizi mbona Vijana siwaoni?
ReplyDeleteNaona wapambe wote na wasindikizaji ni wenye umri wa vijana wa zamani.