Zanzibar Inaweza Kuwa Singapore Ya Pili - Aboud
Asema Hakuna Sababu Z’bar Kuwa Nyuma Kimaendeleo
lUvuvi wa bahari kuu, utalii nyenzo muhimu kufikia kujitegemea
MGOMBEA urais wa Zanzibar kupitia CCM katika uchaguzi mkuu ujao, Mohammed Aboud Mohammed ameahidi kujenga ushindani wa maendeleo kati ya Zanzibar na visiwa vingine kama vile Singapore.
Amesema mazingira ya Zanzibar na Singapore yanalingana na kwamba hakuna sababu ya Zanzibar kuwa nyuma kimaendeleo tofauti na kisiwa hicho.
‘’Maendeleo ya Singapore na visiwa vingine ni mazuri hakuna sababu na sisi tusipige hatua ya maendeleo," alisema Aboud
Alisema kinachohitajika ni ubunifu na kutumia rasilimali ziliopo ili kufikia hatua kubwa kimaendeleo kwa faida ya taifa na wananchi kwa jumla.
Alifahamisha kwamba moja ya rasilimali hizo ni vivutio vya utalii Zanzibar ambavyo vinauwezo mkubwa wa kuibadilisha Zanzibar.
Pamoja na utalii, Aboud alisema bahari ya Zanzibar ina samaki wa kutosha na kwamba ikiwa kipaumbele kitawekwa katika uvuvi wa bahari kuu tunaweza kuanzisha viwanda vya kusindika samaki.
Kuhusu michezo, alisema Zanzibar inasifa ya kuwa na wanamichezo wazuri na kwamba endapo atashinda serikali itajenga chuo cha kufundisha michezo mbali mbali ili kulinda sifa hiyo.
MGOMBEA urais wa Zanzibar kupitia CCM katika uchaguzi mkuu ujao, Mohammed Aboud Mohammed ameahidi kujenga ushindani wa maendeleo kati ya Zanzibar na visiwa vingine kama vile Singapore.
Amesema mazingira ya Zanzibar na Singapore yanalingana na kwamba hakuna sababu ya Zanzibar kuwa nyuma kimaendeleo tofauti na kisiwa hicho.
‘’Maendeleo ya Singapore na visiwa vingine ni mazuri hakuna sababu na sisi tusipige hatua ya maendeleo," alisema Aboud
Alisema kinachohitajika ni ubunifu na kutumia rasilimali ziliopo ili kufikia hatua kubwa kimaendeleo kwa faida ya taifa na wananchi kwa jumla.
Alifahamisha kwamba moja ya rasilimali hizo ni vivutio vya utalii Zanzibar ambavyo vinauwezo mkubwa wa kuibadilisha Zanzibar.
Pamoja na utalii, Aboud alisema bahari ya Zanzibar ina samaki wa kutosha na kwamba ikiwa kipaumbele kitawekwa katika uvuvi wa bahari kuu tunaweza kuanzisha viwanda vya kusindika samaki.
Kuhusu michezo, alisema Zanzibar inasifa ya kuwa na wanamichezo wazuri na kwamba endapo atashinda serikali itajenga chuo cha kufundisha michezo mbali mbali ili kulinda sifa hiyo.
Mzee Mapara,
ReplyDeleteAsante sana kwa hizi picha. Lakini vipi mbona ya Mh Mohd Aboud haipo? au uliishiwa na mkanda? Au kuna neno? Hebu tuekee hili hambo sawa.
Mdau
Samahani si kama mkanda ulikwisha ila hatukupata angle nzuri ya kuweka potrait.
ReplyDeleteHata hivyo picha nyengine zinamuonesha mheshimiwa katika kujitasmbulisha na kujieleza kwa waandishi.
Hakuna neno mdau ni katika kuwakilisha tu
Shukran sana Mzee Mapara. Nakupa hai kwa kazi yako kubwa ya kutumwagia hizi picha quality. Keep it up!
ReplyDeleteMdau
USA