Habari za Punde

Wazee CCM wampongeza Dk. Shein


Na Mwandishi wetu
WAZEE wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar wamempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, kwa kuadhimisha kwa miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wazee hao walisema maadhimisho hayo yalikuwa na mafanikio sambamba na kushuhudiwa hatua kubwa za maendeleo zilizofikiwa katika visiwa vya Unguja na Pemba.


Wazee hao walisema utekelezaji wa kauli ya CCM ya Mapinduzi Daima ilitafsiriwa kwa vitendo kuboresha maendeleo ya nchi na wananchi.

Walisema uzinduzi wa miradi ya  skuli za kisasa, vituo vya afya, uboreshaji wa nyumba za wazee, barabara za kisasa, madaraja, upanuzi wa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji maji, majengo ya afisi za serikali ni hatua moja ya kufikiwa maendeleo hayo.

Aidha walimsifu Dk. Shein kwa kuendelea kusimamia vyema serikali yake yenye mfumo wa umoja wa kitaifa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.