Na
Mwanajuma Mmanga
SERIKALI
imeshauriwa kuanzisha mahakama maalum itakayoshughulikia kesi za dawa za
kulevya kutokana na mahakama zilizopo kuchelewesha kesi za aina hiyo.
Ushauri
huo umetolewa na Mkuu wa kitengo cha kuzuia dawa ya kulevya, Mrakibu mwandamizi
wa Polisi (SSP) Mkadam Khamis Mkadam alipozungumza
na mwandishi wa habari ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar.
Alisema
ucheleweshaji wa kesi hizo umekuwa ni kikwazo kikubwa katika vita dhidi ya dawa
za kulevya kwani watu wengi kuamua kujiingiza katika biashara hiyo kwa kesi
zake zimekuwa zikichukua muda mrefu kutolewa hukumu huku washitakiwa wakibakia
nje.
"Wanapozidi
kuchelewesha kesi za dawa ya kulevya uozo unazidi na watu wengine kushajiishika
kujiingiza katika biashara hiyo," alisema.
Alisema
iwapo mahakama zingeendesha kesi hizo kwa haraka na ushahidi kukamilika na
kutolewa hukumu kungepunguza msongamano wa washitakiwa waliko mahabusu kwa
makosa ya dawa za kulevya.
Mkadam
ameitaka mahakama kuwa na mpango maalum wa usikilizwaji wa kesi na kufuata haki
kama zinavyotakiwa.
Kwa
upande wa wananchi wamelitaka jeshi la polisi kutoa ushirikiano ili kudhibiti
uingizaji, usambazaji na utumiaji dawa za kulevya.
"Jeshi
la polisi halitoi ushirikiano na wananchi wake katika kuondosha biashara hii,”
walisema wananchi hao.
Nae
Naibu Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa
ya jinai Zanzibar, Kamishna Msaidizi wa
polisi,Yusuf J. Ilembo alisema kumekuwepo uharibifu wa makusudi kwa kesi za
dawa za kulevya na kusababisha kwa asilimia kubwa washtakiwa wake kukwepa mkono
wa sheria.
Alisema
vitendo hivyo vinafanywa na watendaji wenye majukumu ya kusimamia utekelezaji
wa sheria.
Alisema
hilo
linachangia kwa kiasi kikubwa uzoroteshaji wa mafanikio ya mapambano dhidi ya
dawa za kulevya kwani wafanyabiashara hao hawana cha kupoteza katika mwendelezo
wa biashara zao haramu.
Takwimu
za dawa ya kulevya zilizoripotiwa katika kipindi cha kuanzia Januari 2010 hadi
11 Oktoba 2012 ni kesi 478, zilizofikishwa mahakamani 422 na zilizokutwa na hatia 31.
Aidha
kesi 95 zilifutwa na mahakama, kesi
zinazoendelea mahakamani 296 na zilizofutwa polisi 32.
Nae
Mrajis wa Mahakama Kuu Zanzibar George Kazi, alisema kuweko kwa mrundikano wa
kesi nyingi mahakamani na kutopatiwa hukumu ni moja ya changamoto zinazoikwaza
mahakama kutoka ofisi ya Mwendesha Mashitaka (DPP) kutokamilisha upelelezi kwa
wakati.
Kwa
mfano alisema mashahidi wa kesi hizo wamekuwa wagumu kufika mahakamani kutoa
ushahidi, hali inayozifanya kesi hizo kuchukua muda mrefu kupatiwa hukumu.
Aidha
alisema kuna kesi nyingi katika ofisi ya Mkemia Mkuu wa serikali zinazosubiri
ushahidi wa kitaalamu kama vile vipimo vya
mkojo.
No comments:
Post a Comment