Habari za Punde

Afikishwa Mahakamani akituhumiwa kuiba Magodoro

Na Maryam Salim, Pemba.
MSHITAKIWA, Khamis Said Ramadhan ( 28) mkaazi wa Vikutani- Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba ,amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Chake Chake kujibu shitaka lake la kuvunja na kuiba magodoro 4 katika Chuo cha Mafunzo ya Amali Vitongoji .
Kwa upande wa hati ya Mashtaka iliyowasilishwa Mahkamani hapo , ulidai mbele ya  Hakimu, Omar Mcha Hamza, kuwa siku ya Jumamosi muda usiojulikana ya  Agosti 25 mwaka huu, alitenda kosa hilo huko katika chuo cha Mafunzo ya Amali Vitongoji ikiwa ni  Mali ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar .
Mshitakiwa huyo ilidaiwa kuwa aliiba magodoro 4 ya futi sita kwa sita yenye thamani ya T.sh,360,000/=kwa makisio mali ya kituo cha mafunzo ya Amali kilichipo Vitongoji .
Muendesha mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, Seif Mohammed Khamis, alidai Mahakamani hapo kuwa Mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo ikiwa ni kosa K/F cha sheria NO.6/2004 sheria ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Kwa upande wa mashahidi 6 ambao ni, Ayoub Magawe Habira ,Juma Mussa Ame,Juma Suleiman Saleh ,Salim Ali Mbarouk ,Fatma Ali Khamis na D3399 D/C sajent Juma ,tayari walishapandishwa na kutoa ushahidi juu ya tuhuma hizo.
Mashahidi hao walidai kuwa, mshitakiwa huyo hawakumuona kuvunja wala kuiba bali walipata taarifa kutoka kwa mnunuzi, ambaye ni Salim Ali Mbarouk alidai kuwa aliuziwa Godoro moja kutoka kwa kijana huyo kwa bei ya Tsh,5000/= bila ya ushahidi bila risiti kutoka kwa muuzaji, kwa sababu alimueleza kuwa anashida.
 Khamis Said Ramadhan, alipotakiwa kujibu shitaka lake,  mahakamani hapo alikana  ushahidi uliotolewa na Askari Upelelezi, kwani siku hiyo alidai hakuwepo katika eneo la tukio ,na kuiambia Mahakama kwamba Magodoro yaliyoibiwa ilidaiwa ni 4, lakini  lilikamatwa ni moja, aliiuliza mahakama hiyo na kuiomba mahakama iyangalie kwa vyema ushahidi ambao umetolewa.
Baada ya maelezo hayo Hakimu Omar Mcha Hamza aliihairisha kesi hiyo hadi Septemba 11mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.