Habari za Punde

Mahakamani kwa kubaka Mapacha

Na Laifat Kassim, Pemba.
MAHAKAMA ya mkoa wa Chake Chake, imempandisha katika Kizimba cha Mahakama , Abubakar Mkulu Bakar [28] mkaazi wa Wambaa, Mkoa wa Kusini Pemba, kujibu tuhuma ya kuwabaka watoto wawili wa kike [13] kila mmoja ( Mapacha)  wakaazi wa Msuka Mtoni Wilaya ya Micheweni.
Kitendo hicho kilichofanywa na mtuhumiwa huyo  ni kosa kwa mujibu wa kifungu cha 125 [1] [2] [e] na K/F cha 126 [1] cha sheria namba 6 ya mwaka 2004 sheria ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa hati za mashtaka iliyowasilishwa Mahakamani hapo na Muendesha mashtaka kutoka Ofisi ya mkurugenzi wa Mashtaka, Ali Bilali Hassan, mbele ya Hakimu, Khamis Ramadhani  Abdalla, mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo, baina ya mwaka 2011 na mwaka 2013 huko Wambaa Mkoani Pemba, Tanga na Mwanza -Tanzania Bara kwa makusudi ambapo  aliwabaka watoto hao na kuwasababishia maumivu sehemu ya siri, jambo ambalo ni kosa kisheria.

Baada ya kusomewa waraka huo, Mshtakiwa alikataa kuwafanyia kitendo hicho isipokuwa alikiri kuwa Watoto hao alikuwa nao.  
“Mimi toka niwachukue watoto hao sijawahi kuwafanyia hata siku moja kitu hicho na nilikuwa ninawalea kama watoto wangu niliwowazaa”alisema .
Kwa upande wa Shahidi namba moja ambae ndie baba wa mapacha hao mkaazi wa Msuka, alidai kuwa aliwachukuwa  kwani alimpa watoto wake   wakati yeye  akiwa ni Mgonjwa.
“Kwa kweli kijana huyu aliizoea kwangu nakuniambia ni Mganga wa kutengeneza dawa, kwa vile nilikuwa ni mgonjwa wa vidonda vya tumbo alinitengenezea Dawa nikanywa, baada ya kunywa maradhi yalizidi na kuondoka na watoto wangu”  alidai.
Alidai baada ya kuondoka na watoto hao alikuwa anawasiliana naye  na baadae mawasiliano yakakatika kwa muda wa miezi sita[6] na baadae aliamua kumfuatilia mshtakiwa huyo kwenda Tanga kuwaona watoto wake ingawa hakufanikiwa.
“Baada ya kushauriana na mke wangu na kujenga wasiwasi mkubwa kwa watoto wangu niliuza ng’ombe na kwenda Tanga kuwachukuwa watoto wangu nilipofika simu ikazimwa na sikuipata tena, niliwatafuta lakini sikuwaona nikarudi” alidai.
Kwa upande wa shahidi namba mbili ambae ni baba mdogo wa mapacha hao aliiambia mahakama kuwa, mtuhumiwa huyo baada ya kukamatwa na kupelekwa Polisi na baadae kwenda Hospitali kwa ajili ya vipimo vya watoto hao na kuonekana wameharibiwa alimwambia kuwa, yalopita yamepita, hivyo nakuomba unisamehe.
“Baada ya kipimo kuonesha watoto wameharibiwa, aliniambia nimsamehe na ataniandikia kipande cha shamba au atanipa pesa ninazotaka”Alieleza.
Baada ya ushahidi huo nao kati wa mapacha hao  ambae ni shahidi namba tatu alidai kuwa, nikweli alikuwa anawafanyia uovu huo, na kabla ya kuwafanyia alikuwa anajipaka mafuta au mate katika sehemu zake za siri na baadae kuwaingiliza sehemu za siri za mbele kwa zamu.
“Sisi alikuwa anatuambia tuende Kisimani na mmoja abakie na nikibakia ananivua nguo na kunifanyia udhalilishaji huo na alikuwa anatufanya kwa zamu na akimaliza alituambia tusiseme” Alieleza Shahidi huyo.
Nae shahidi namba nne ambae ni mmoja kati ya mapacha hao, aliiambia mahakama kuwa, alikuwa anawambia yeyote ambae atawauliza waseme kuwa ni baba yao wa kuwazaa na kama hawakusema alikuwa anawapiga.
“Kila ambae anatuuliza tulikuwa tunasema ni baba yetu alotuzaa na siku ambayo tumekosea hatukusema hivyo akisikia alikuwa anatupiga bakora” alisema Shahidi huyo.
Baada ya ushahidi huo, mshtakiwa alijitetea na kuiambia Mahakama anaomba dhamana, lakini Hakimu wa Mahakama hiyo, alimuambia kama atapata wadhamini madhubuti ataweza kupata dhamana na kabla ya dhamana awe na Shilingi milioni moja [1000,000/=] taslimu na wadhamini wawili.
Kesi hiyo imehairishwa hadi Juni 5 mwaka huu kwa kuwasikiliza mashahidi wengine, ambapo Mtuhumiwa huyo alirudishwa Rumande.

2 comments:

  1. asipewe dhamana wala waraka huyo anastahili afungwe tena kifungo cha miaka isiopungua 40 ili akitoka asiwe na nguvu ya kudhalilisha watoto wetu wengine.. mtovu wa adabu asokua na adabu... mjaalana mkubwa....

    ReplyDelete
  2. Subhanallah lakini watu wataacha lini mambo haya ya kuaminiana mpaka kumpa mtu watoto wako .
    ' No country for oldmen '

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.