Na
Asha Salim, Pemba
KIJANA Haroub Muhamed Hamad (22) mkaazi wa Ole Kianga
apatiwa onyo la mwisho katika Mahkama ya wilaya Chake chake kwa kosa la kukataa
kufahamu utaratibu wa mahkama chini ya hakimu Omar Mcha Hamza.
Ilionekana mahakamani hapo kuwa, mtuhumiwa
alikuwa na ubishani kwa kila anachofahamishwa ,kuhusiana na vielelezo ambavyo
vimefikishwa mbele ya mahkama, kwa ajili ya uthibitisho wa tuhuma ambazo
zinamkabili juu yake mahakamani hapo.
Awali, mwendesha mashtaka kutoka ofisi ya
mkurugenzi wa mashtaka, Seif Muhamed Khamis, aliiambia mahkama kuwa, shauri
lililetwa mezani kwa ajili ya kusikilizwa na ushahidi utatolewa kwa upande wa upelelezi juu ya mtuhumiwa.
Shahidi wa upelelezi kutoka upande wa
mahkama F 6368 D/C, Yussuf( 30), aliieleza mahkama kuwa wakati akiwa katika kituo chake cha kazi Polisi
Madungu, alipewa taarifa na Mkuu wake kuwa, kuna tukio la wizi wa Ng’ombe atoke
na wenzake kwenda eneo husika kupata taarifa .
Alidai
walikwenda eneo la tukio, ambapo walimkuta raia huyo, Suleiman Khamis, ambae alitoa taarifa za
mwanzo, pamoja na mtuhumiwa akiwa na Ng’ombe, aliekusudia kumuuza bila ya
kuhitaji shahidi, akidai kuwa ni wa familia na hahitaji itambue taarifa yoyote.
Aliendelea kudai mahakamani hapo kuwa, walimchukua mtuhumiwa
pamoja na Ng’ombe kumpeleka Kituoni , na mara baada ya kumuhoji alionekana
kubadili majibu na kusema kuwa amemuokota mabondeni, hamjui mwenyewe wakati
mwanzo alieleza ni wa familia.
Baada ya ushahidi huo Hakimu pia alimtaka
mtuhumiwa kuthibitisha ushahidi wa hati ya maelezo ambayo aliyatoa mwenyewe
wakati alipokuwa akichukuliwa maelezo katika mahkama ya mwanzo Chake
chake, chini ya Hakimu, Thubeit na kuonekana kwamba alikiri kutenda kosa hilo.
“Muheshimiwa hakimu nina pingamizi na
kielelezo kilichofikishwa mbele ya Mahkama yako, kwasababu mimi naaambiwa
nimeiba wakati Ng’ombe kapewa mlalamikaji amtunze, hakuachwa Mahkamani usipokee
kielelezo hicho” alidai mtuhumiwa.
Aidha alidai kuwa , yeye hata akioneshwa
vielelezo vyote hafahamu chochote na kwamba hahitaji mashahidi wanaopokea
taarifa za kusikia , hali ambayo ilionekana kusababisha upinzani mkubwa baina
yake na hakimu mahkamani hapo.
“Kuletwa mbele ya mahkama kujibu tuhuma
, haijulikani kwamba tayari wewe ni mfungwa wa kosa ,waache mashahidi wote
waitwe wakimaliza, mahkama itaangalia uwamuzi juu ya kuthibitika kwa kosa au
laa ndio maana ya kuitwa mashahidi ,kwanini unaleta ushindani kwa kila
unachofahamishwa” alisema Hakimu.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, iliyowasilishwa
mahkamani hapo, ilidai kuwa mnamo siku ya Aprili 16, 2012 majira ya saa 10:00
jioni mtuhumiwa aliiba Ng’ombe jike mwekundu mwenye thamani ya Tsh,300,000 maneo
ya Mbuzini Chake chake Pemba ,ambapo ni kosa kif, 267(1) na
274(1)(2)(C) sheria no.6/2004 sheria ya Zanzibar.
Nae, mwendesha mashtaka alimuomba Hakimu
kupokea kielelezo cha maandishi ya maelezo ya mtuhumiwa iwe kama ni ushahidi
utakaosaidia mahkama pamoja na picha ambazo, zilitolewa kueka kumbukumbu ya
kukabidhiwa Ng’ombe, kwa ajili ya matunzo kwa mlalamikaji.
“Muheshimiwa hakimu ,shauri litaendelea kusikilizwa
shahidi ambae ni Hakimu , aliyemchukulia maelezo kwa ajili ya ushahidi zaidi
shahidi huyo leo hayupo hivyo naomba ipangiwe tarehe nyengine”aliema muendesha
mashtaka.
Hakimu aliakhirisha shauri hilo hadi juni ,24 mwaka
huu kwa kusikilizwa shahidi.
No comments:
Post a Comment