Habari za Punde

Kamati Bunge la Katiba hadharani leo

Na Mwantanga Ame
WAJUMBE wa Kamati 12 za bunge maalum za katiba wanatarajiwa kutangazwa leo.
Mwenyekiti wa bunge hilo,  Samuel Sitta, anatarajiwa kutangaza kamati hizo ikiwa ni sehemu ya kazi zilizopangwa kutekelezwa baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete kulizindua rasmi bunge hilo.
 Kabla ya kuifanya kazi hiyo, Sitta  anatarajiwa kuendelea kuwaapisha wajumbe wengine ambao bado walikuwa hawajaapishwa.
Uundwaji wa kamati hizo ni sehemu ya utekelezaji wa kanuni za bunge hilo amabalo lilipendekeza kuundwa kwa kamati 12 ambazo zitatumika kupitia rasimu hiyo na baada ya kukamili kuwasilisha mapendekezo yao

 Wakati hatua hizo zikiendelea vyombo vya habari havitaruhusiwa kuingia katika kamati hizo wakati wajumbe wakiendelea na mjadala wao, na badala yake vitalazimika kupata taarifa hizo baada ya kumalizika kupitia Mwenyekiti wake. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.