Habari za Punde

Hutuba ya Utilianaji Saini Mradi wa Uhifadhi wa Urithi wa Zanzibar na Kutengeneza Ajira.

untitled1

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

12th APRILI, 2014.
 
Ndugu Makamo Mwenyekiti wa JUHIMKO,
Wajumbe wa Baraza JUHIMKO,
Msimamizi Mkuu wa Jumuiya ya ACRA Nchini Tz,
Meneja wa Mradi,
Wanachama wa JUHIMKO,
Wageni Waalikwa,
Ndugu waandishi wa habari,
Mabibi na Mabwana

Assalaam Alaykum,
Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukusanyika hapa leo hii.  Hivyo nachukua nafasi hii kutoa shukurani zangu kwenu nyinyi wote mliohuduria katika shughuli hii ya kutiliana saini za makubaliano ya utekelezaji wa Mradi wa pamoja  baina ya Jumuiya ya Hifadhi Mji Mkongwe na Jumuiya ya ACRA.

JINA LA MRADI:  Uhifadhi wa Urithi wa Zanzibar na Kutengeneza ajira. (Zanzibar Built Heritage for job creation)

MUOMBAJI WA MRADI: ACRA

WASHIRIKA WA MRADI:  ZSTHS (JUHIMKO), ACRA & AGSS.

ENEO LA MRADI:  ZANZIBARTANZANIA.

MUDA: MIAKA MITATU.

GHARAMA ZA MRADI: EURO 1,200,000/=

LENGO LA MRADI: Mradi huu una lengo la kuhifadhi, kutunza na kuutangaza urithi wa kiutamaduni uliopo Zanzibar na kuifanya sekta hii kuchangia ukuwaji wa uchumi wa Nchi.

WALENGWA WA MRADI: Jumla ya watu wapatao 15,922 watafaidika na Mradi huu, wakiwemo mafundi ujenzi/waashi 400, watu wasio na ujuzi 75, wajasiria mali katika sekta ya ujenzi  na  ambao wamesajiliwa 22, wamiliki wa majengo ya umma na majengo binafsi 150, watembeza watalii wapatao 50, walimu wa  skuli za msingi na Sekondari 200, wanafunzi wa skuli za msingi na sekondari wapatao 10,000, pamoja na wananchi wa kawaida 5,000 ambao watashirirki katika mikutano na maonyesho mbali mbali.

SHUGHULI ZA MRADI: Mradi huu utajumuisha shughuli zifuatazo;
1.      Kutoa mafunzo ya muda mfupi kuhusiana na matengenezo ya majengo ya kiasili kwa watu wenye ujuzi na wale wasio na ujuzi.
2.      Mradi pia utasaidia kuanzishwa kwa maabara katika Chuo Kikuu cha Taifa SUZA, ambapo maabara hiyo itasaidia kufanyia utafiti unaohusiana na mali ghafi zinazotumika kujenga majengo ya kihistoria.
3.      Mradi utasaidia kuandikwa kwa mtaala unaohusiana na kuyafanyia matengenezo majengo ya kale ambapo mtaala huo utatumiwa na Chuo cha Karume (Karume Institute of Science and Technology).
4.      Kuandaa na kufanya mikutano na wadau mbali mbali kuzungumzia masuala ya urithi wa rasilimali za Kiutamaduni yakiwemo majengo ya asili yaliyopo Zanzibar.
5.       Kutoa mafunzo kuhusiana na masuala ya kufuata taratibu za uhifadhi wa majengo ya kihistoria kwa wajasiriamali pamoja na watu wanaomiliki majengo binafsi na majengo ya umma.
6.      Kutoa mafunzo yanayohusiana na masuala ya urithi kwa walimu, wanafunzi pamoja na jamii yote kwa jumla.


MATOKEO YA MRADI: Mara baada ya kukamilika utekelezaji wa mradi huu, ni matarajio yetu kupata yafuatayo;

i.        Mradi utaweza kusaidia kuongeza ujuzi na ufanisi kwa mafundi pamoja na watu wasio na ujuzi kwa kufanya kazi zao, huku wakizingatia mbinu na taratibu sahihi za kiasili zinazotumika katika ujenzi na uhifadhi wa majengo ya kihistoria.
ii.      Mradi utaweza kukisaidia Chuo Kikuu cha SUZA kwa kuanzisha maabara ambayo itasaidia kufanya shughuli mbalil mbali za kiutafiti unaohusiana na mali ghafi zinazotumika kujenga majengo ya kiasili/kihistoria.
iii.    Mradi utaweza kusaidia Chu cha Karume (Karume Institute of Science and Technology) kupata mtaala unaohusiana na kuyafanyia matengenezo majengo ya kale.  
iv.    Pia mradi utaweza kuwajengea uwezo wadau mbalil mbali katika sekta ya utalii wakiwemo watembezaji watalii, hii itapelekea kutoa taarifa sahihi kwa wageni na wenyeji zinazohusiana na historia pamoja na urithi tulionao.
v.      Vile vile mradi utasaidia sana kuwajengea uwezo na uelewa wa kina kwa walimu, wanafunzi pamoja na jamii kwa ujumla kuhusiana na historian a urithi uliopo katika Nchi yao.

NAFASI YA JUMUIYA YA HIFADHI MJI MKONGWE KATAIKA UTEKELEZAJI WA MRADI:    

Kimsingi Jumuiya ya Hifadhi Mji Mkongwe ni mshirika mwenyeji katika utekezaji wa mradi huu (Local Project Partner), ambapo Jumuiya itatakiwa kutekeleza majukumu yote kama ilivyo katika hati ya makubaliano baina ya yetu na Jumuiya ya ACRA. Miongoni mwa majukumu hayo ni kama ifuatavyuo;
i.        JUHIMKO ndio atakayekuwa muhusiuka mkuu katika kupanga na kutekeleza shughuli mbali mbalil zinazohusiana na kutoa taaluma na kukuza uelewa  juu ya masuala ya kihistoria na urithi wa kiutamaduni uliopo Zanzibar.
ii.      Pia JUHIMKO ndi itakayoandaa mtaala utakaotumika katika shughuli za kutoa taaluma na elimu ya kihistoria pamoja na umuhimu wa kuwa katika ramani ya urithi wa dunia kwa walimu wa skuli mbali mbali za Zanzibar.   
iii.    Kuandaa na kufanya kampeni, katika skuli mbali mbali zenye lengo la kutoa taaluma kwa ajili ya kutoa muamko na kukuza uelewa juu ya masuala ya urithi wa kiutamaduni uliopo Zanzibar na kwengineko, ambapo Jarida la UNESCO linalojuilikana kwa jina la (UNESCO Young Peoples World Heritage Education Programme) litatumika pamoja na kutumia uzoefu kutoka kwa JUHIMKO.  

Ahsanteni kwa kuniskiliza.

TAFSIRI YA UFUPISHO WA MANENO.

ACRA: Cooperazione in africa e America Latina

AGSS: Associazione Giovanni Secco Suardo

ZSTHS: Zanzibar Stone Town Heritage Society.

JUHIMKO: Jumuiya ya Hifadhi Mji Mkongwe.

SUZA: State University of Zanziabar.

Address: Mizingani Road, Old Customs House, P.O. Box 3892 ZanzibarTANZANIA
Phone: +255 (0)24 2237072, e-mail: info@zanzibarstonetown.org, web site: www.zanzibarstonetown.org or
www.stonetownheritagesociety.wordpress.com face book: www.facebook.com/zsths


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.