Habari za Punde

Mapete apigwa ‘stop’ kujimilikisha eneo la soko Wete

Na Abdi Suleiman, Pemba
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, amewataka wafanyabiashara katika soko la Wete kuendelea na biashara zao, licha ya mfanyabiashara mmoja maarufu, Ahemd Abdalla (Mapete) kudai anamiliki eneo hilo.

Alitoa kauli hiyo, baada ya kusikiliza pande zinazovutaka katika mgogoro huo, ambazo kila upande unadi kumiliki eneo lililpo soko hilo.

Pande zinazovutana ni serikali ya mkoa wa kaskazini Pemba na mfanyabiashara huyo maarufu mjini Wete na kisiwani Pemba.

Alisema serikali ndio itakayotoa jibu juu ya mgogoro wa eneo hilo ambalo kwa sasa liko chini ya baraza la mji Wete.

Alimtaka mfanyabiashara huyo anaedai kuuziwa eneo hilo na Katibu wa baraza la mji, ambaye kwa sasa ni marehemu kujua kwambwa wote wana makosa kwani wameuza na kununua mali ya serikali.

 “Eneo hili ni mali ya serikali, limekabidhiwa baraza la mji Wete, sasa huyo mtu aliyekuuzia yeye kafanya makosa na wewe umefanya kosa, kwani mumeiba mali ya serikali,”alisema.

Alisema kwa sasa suala hilo linashughulikiwa na serikali, hadi pale itakapotoa kauli nani mmiliki halali wa eneo hilo, hivyo alimtaka mfanya biashara huyo kutokulitumia kwa kazi yoyote eneo hilo.

Kwa uapande wake, Katibu wa baraza la mji Wete, Faki Hamad Faki, alisema eneo hilo ni mali ya serikali tokea Mapinduzi ya 1964.


Alisema hakuna nyaraka zozote zinazothibitisha kwamba Mapete ameuzia eneo hilo na aliekuwa Katibu wa baraza hilo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.