Habari za Punde

Uchunguzi wa Majina, Majimbo ni matakwa ya Kikatiba

Na Bakar Mussa, Pemba
 
Uchunguzi wa Majina , Idadi wa Watu, majina na Mipaka ya Majimbo ya Uchaguzi Zanzibar, unaotarajiwa kufanywa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar,   ni matakwa ya Kikatiba ambayo yalianza kwa muda mrefu uliopita, pamoja na Tume hiyo kuchelewa kufanya hivyo.
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salim Jecha,huko katika Ukumbi wa Hoteli ya Hifadhi Pemba, wakati alipokuwa akizungumza na Wadau wa Uchaguzi wakiwemo Viongozi wa Vyama vya Siasa , Taasisi za Serikali, na Wadau wengine juu ya matagemeo ya Tume  ya kufanya hivyo.
Mwenyekiti huyo , alisema kuwa ili kufanya kazi hiyo , mashirikiano ya pamoja yanahitajika kwa kila mmoja ili kuweza kufanyika kwa kazi hiyo muhimu kama Katiba ya Zanzibar inavyoelekeza kifungu cha 120 cha Katiba.
“ Kazi tunayoitarajia kufanya sisi Tume ya Uchaguzi (ZEC), si matakwa yetu bali ni Katiba ya Zanzibar , ndio inayotuelekeza kufanya hivyo pamoja na kwamba tumechelewa,”alieleza Mwenyekiti.

Nae,Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (ZEC),Salim Kassim Ali, alisema kuwa ili kuweza kuifanikisha kazi hiyo muhimu kwa Taifa inategemea kupata maoni ya Wadau waliomo katika Majimbo ya Uchaguzi kama ilivyohivi sasa katika Wilaya mbali mbali za Unguja na Pemba.
Alifahamisha kuwa ili kuweza kufanikisha vyema kazi hii Tume ya Uchaguzi Zanzibar, imeandaa utaratibu maalumu wa kukusanya Maoni hayo juu majimbo kwa taasisi na  Watu ambao  hawatapata nafasi ya kutowa maoni yao katika mikutano hiyo wanaweza kutowa maoni yao kwa maandishi.
Aidha , alisema kuwa Tume ya Uchaguzi inatarajia kulieka Wazi Daftari la Kudumu  la Wapiga kura katika Majimbo yote ya Uchaguzi Zanzibar, kuanzia tarehe 21 hadi 26 /6 mwaka huu, ili kupata maboresho ya Daftari hilo na kueka sawa ili kuondosha malalamiko yasiokuwa ya lazima.
Ayoub Bakar Hamad, Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC),itaendelea kuwashirikisha Wadau wake wa Uchaguzi kwa kila jambo linalohusiana na Uchaguzi , kwa kufanya  hivyo ni kupanuwa wigo wa Demokrasia nchini, na hilo litakalofanyika ni matakwa ya kikatiba na kamwe sio matakwa ya Tume hiyo.
Alieleza kuwa Tume ya Uchaguzi itazingatia na uzito uzito wa hoja za msingi na sio idadi ya watu watakao towa maoni yao , nan i vizuri maoni yakitolewa kwa maandishi ambayo ytasaidia Tume hiyo katika kufanya uhakiki wake vizuri na kwa Uwazi.
“ Taasisi zitazopata fursa ya kutowa maoni hayo ni vyema wakatowa yaliofananakwa pamoja ili kuondowa mgongano katika Taasisi zao,” alieleza, Mjumbe huyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.