Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi-Zanzibar
(ZEC),Salim Kassim Ali, akitowa maelezo juu Mkutano wa Wadau wa Uchaguzi na
Tume juu ya Ugawaji wa Majimbo Zanzibar.
Wanasiasa wa Vyama mbali mbali wakifuatilia
kwa makini madhumuni ya Mkutano wa Tume ya Uchaguzi na Wadau huko katika Hoteli
ya Hifadhi Chake Chake Pemba.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC) Jecha
Salim Jecha, akifunguwa mkutano wa Wadau wa Uchaguzi huko katika Hoteli ya
Hifadhi Chake Chake Pemba.
Wakuu wa Mikoa miwili ya Pemba, Meja
Mstaafu Juma Kassim Tindwa, na Dadi Faki Dadi, wakisikiliza kwa makini
madhumuni ya Mkutano wa Tume na Wadau wa Uchaguzi Kisiwani Pemba.
Mratibu wa Chama cha CHADEMA, Pemba,
akitowa maelezo juu ya mashirikiano madogo baina ya Tume na Chama chake, huko
katika Hoteli ya Hifadhi Kisiwani Pemba.
hivi visiwa vyote ukivikusanya ukubwa wake haufikii hata nusu ya Dar es salaam , sasa sielewi hivi kutaka kuongeza majimbo kuna umuhimu gani kama sio kuongeza gharama na mzigo kwa wananchi wenye kulipa kodi , ukiongeza majimbo maanake utaongeza ruzuku za uchaguzi kwa vyama , gharama za kuendesha chaguzi , mishahara na marupurupu atayolipwa huyo mwakilishi /mbunge watakaechaguliwa , kama watu hatuna akili za kuzaliwa basi tutumie angalao tulizopata skuli
ReplyDelete