Bajeti ya Wizara ya Afya ambayo ilikuwa inajadiliwa katika Mkutano wa bajeti unaondelea
imerejeshwa tena katika Kamati ya Maendeleo ya Wanawake na Ustawi wa Jamii , kwa ajili ya marekebisho zaidi.
Spika wa Baraza la Wawakilishi
Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho amesema,
Baraza la Wawakilishi limefikia uwamuzi
huo baada ya Wajumbe wengi kubaini mapungufu makubwa ya mgawanyo wa fedha katika
bajeti ya Wizara hiyo mwaka huu.
Spika Kificho ametowa ufafanuzi huo
leo wakati akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini kwake Chukwani.
Amesema Wajumbe hao sio tu wamebaini
kiasi kidogo cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya wizara hiyo mwaka huu, bali pia
maeneo ambayo sio kipaumbele cha Wizara yametengewa fedha nyingi
ukilinganisha na maeneo ya kutoa huduma
ambayo yametengewa kasma ndogo mno kiasi ambacho kitanguza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa
jamii kwa kiwango kikubwa.
Kwa hatua hiyo Mheshimiwa Spika
ameagiza bajeti hiyo irudi katika Kamati
husika ili ikae tena na Wizara ya Afya
pamoja na Watendaji wa Wizara ya Fedha kwa
lengo la kurekebisha mapungufu hayo kabla ya kuendelea kujadiliwa tena ndani ya
Baraza Jumanne ijayo.
Tukio hili linaonyesha jinsi Wajumbe
wa Baraza la Wawakilishi walivyo makini
katika kuhakikisha bajeti ya Serikali
inakuwa kwa maslahi ya wananchi na si vinginevyo.
Hivi karibuni, Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi walipatiwa mafunzo kuhusu
uchambuzi wa Bajeti kupitia mradi wa Kuimarisha Vyombo vya Kutunga sheria (LSP)
na umakini huo wa Wajumbe katika kuijadili Bajeti ya Wizara ya afya
unathibitisha namna mafunzo hayo yalivyosaidia katika kuwajengea Wajumbe uwezo
katika eneo hilo la kujadili na kupitisha bajeti.
No comments:
Post a Comment