Na
Husna Mohammed
SERIKALI
ya Mapinduzi Zanzibar, imesema licha ya kwamba hati ya Muungano haikuridhiwa na
Baraza la Mapinduzi, lakini muungano huo ni halali.
Mwanasheria
Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman,aliliambia baraza la wawakilishi jana
wakati akijibu hoja za wajumbe wa baraza hilo
waliochangia hotuba ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2014/2015.
Alisema
kutoridhiwa kwa hati hiyo ya muungano hakubatilishi muungano wa Tanganyika na Zanzibar .
“Muungano
wa Tanganyika na Zanzibar ni halali na kwa kuwa hati hiyo haikuridhiwa basi
bado haijabatilisha muungano kwa mujibu wa sheria,” alisema.
Akizungumzia
kuhusu umiliki wa kisiwa cha Fungu Mbaraka, Mwanasheria huyo alisema kisiwa
hicho ni milki ya Zanzibar .
Alisema
kisiwa hicho kinamilikiwa na Zanzibar
na hadi sasa hakuna mtu au taasisi
yoyote iliyodai kumiliki kisiwa hicho.
"Tumeangalia
katika utaratibu wa sheria hakuna madai ya umiliki wa kisiwa hicho kwa mtu au
taasisi yoyote nataka kuithibitishia serikali na watu wake," alisema.
Alisema
kisiwa hicho kinamiliwa na Zanzibar
tokea mwaka miaka 1918 ambapo kilirithiwa kutoka kwa Ujerumani.
Alisema
madai ya kusema kisiwa hicho si mali
ya Zanzibar hayana msingi wowote hasa kutokana
na kuweko kwa mikataba na sheria inaonesha ni haki ya Zanzibar .
"Serikali
inatoa agizo rasmi kwa wizara husika kuandaa mipango madhubuti ya kukiendesha
kisiwa hicho kwa sababu hadi sasa hakuna madai yoyote kuhusiana na kisiwa
hicho,” alisema.
Kuhusu
Tume ya pamoja ya Fedha, alisema kuanzisha kwa akaunti ya fedha za pamoja ni
muhumu kwani ibara ya 133 inaeleza wazi kuwa akaunti hiyo ndio inayoweka fedha
za muungano.
"Kuweko
kwa akaunti hiyo kwa kiasi kikubwa kutaondosha hata mzozo wa muungano na itatumiwa na wote na kuweka mipaka kati ya
mamlaka ya Serikali ya Muungano na ile ya Tanzania Bara,” alisema.
No comments:
Post a Comment