Habari za Punde

DW chatoa mafunzo kwa wakufunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari

Khadija Khamis na Rahma Khamis, zjmmc  
 
Kituo cha Mafunzo cha DEUTSCHE WELLE (DW)kimeendelea kutoa Mafunzo kwa Wakufunzi wa Chuo cha Uandishi habari wa Zanzibar ikiwa ni mwendelezo wa Mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Ujerumani.
 
Mafunzo hayo ya siku tano yana lengo la kuwajengea uwezo Wakufunzi wa Chuo hicho ili kutoa elimu sahihi ya Uandishi inayoendana sambamba na mabadiliko ya kiulimwengu.
 
Akizungumza na waandishi wa habari hizi huko ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar Kaimu Mkuu wa Chuo hicho Rashid Omar Kombo alisema Wataalamu hao watawajengea uwezo Wakufunzi wao ili kusaidia katika kufundisha wanafunzi kwa vitendo na kutumia njia za kisasa katika ufundishaji wao.
 
Omar amefahamisha kuwa mafunzo hayo ya vitendo kwa darasa (compelete class training) yatasaidia kutoa mbinu kwa Uandishi wa habari  wa kileo ambao unakwenda sambamba  na matarajio ya wana jami.
 
Ameongeza kuwa licha ya kupatiwa mafunzo pia wanatarajia kupatiwa misaada ya vifaa mbalimbali vya ufundishaji ikiwemo Camera na Komputa pamoja na kujenga majengo mbali mbali ya Chuo katika maeneo mengine.
 
Aidha aliongeza kuwa mafunzo hayo ni mwendelezo wa Mafunzo ambayo hutolewa na Kituo hicho cha DW kwa Chuo cha Habari ambapo Mwanzoni mafunzo hayo yalitolewa kwa wanafunzi tu wa chuoni hapo.
 
Jumla ya Wakufunzi 16 wa Chuo cha Habari Zanzibar wanaendelea kupatiwa mafunzo hayo kutoka kwa Wataalamu watatu wa kituo cha Mafunzo cha DW ambayo yatachukua siku tano.
 
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.