Habari za Punde

PBZ Yakabidhi Fulana kwa Ajili ya Maadhimisho Miaka 50 ya Elimu Bila Malipo Zanzibar.

Kaimu Mkurugenzi Masoko wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Ndg. Seif Suleiman akiwa na moja ya fulana zilizotolewa na PBZ kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Elimu bila malipo yanayotarajiwa kuadhimishwa 23.9,2014 katika viwanja vya Amaan Zanzibar. Kulia Mkurugenzi Idara ya Maandalizi na Msingi Bi Safia Ali Rijali. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi ya Idara ya Maandalizi na Msingi Mazizini Zanzibar.
Kaimu Mkurugenzi Masoko wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Ndg. Seif Suleiman akimkabidhi fulana Mkurugenzi Idara ya Maandalizi na Msingi Bi Safia Ali Rijal kwa ajili ya maadhimisho ya Tamasha la miaka 50 ya Elimu Bila Malipo yanayotarajiwa kuadhimishwa wiki ijayo katika viwanja vya Amaan Zanzibar. .

 Mkurugenzi Idara ya Elimu Maandalizi na Msingi Bi Safia Ali Rijal. akitowa shukrani kwa niaba ya Wizara ya Elimu kwa Uongozi wa PBZ kwa msaada wao kufanikisha Tamasha la Elimu Bila Malipo linalotarajiwa kuadhimishwa wiki ijayo, Amesema Elimu Bila Malipo inamgusa kila Mtu katika Zanzibar,   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.