Habari za Punde

TEACA yagawa mizinga ya nyuki

Na Kija Elias, Moshi
KATIKA kukabiliana na matukio ya uharibifu wa mazingira mkoani Kilimanjaro,  Shirika lisilo la  kiserikali linalojishughulisha na utunzaji na uhifadhi wa mazingira (TEACA), limekabidhi mizinga 50 yenye thamani ya shilingi milioni 4.2 kwa mtandao wa hifadhi ya msitu wa nusu maili Kilimanjaro (KIHACONE).

Akikabidhi mizinga hiyo, Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Adoncome Mcharo, alisema uhamasishaji wa ufugaji wa nyuki utawezesha kuondoa uvunaji ovyo wa misitu kwenye maeneo ya hifadhi na kwamba wananchi hao  watajikita katika shughuli za ufugaji wa nyuki.

Alisema mpango huo wa kuwapatia mizinga hiyo, utawawezesha wananchi kuwa na elimu ya utunzaji wa mazingira, pamoja na kupata njia bora ya kisasa ya uvunaji  wa asali  bila kutumia  moto.

Kwa upande wake, Mbunge wa viti Maalumu CCM,  Dk. Bethy Machangu, alisema ufugaji wa nyuki unaweza kubadili na kumkomboa mwananchi wa kipato cha  chini endapo utapewa kipaumbele.


Alisema silaha kubwa ya kupambana na umasikini ni kuwekeza kwa vijana na wanawake kuwa na ufanisi katika ufugaji wa nyuki.

Awali akipokea mizinga hiyo, Mwenyekiti wa mtandao wa vijiji 37, vinavyozunguka mlima Kilimanjaro, Boniface Mbando, alisema mizinga hiyo itafungua njia kwa wananchi kuwekeza 
zaidi katika ufugaji wa nyuki.


Mtandao huo umekabidhi  mizinga 50 kwa vijiji 10 vinavyozunguka hifadhi ya mlima Kilimanjaro, lengo likiwa ni kuhakikisha mikakati waliojiwekea.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.