Na Tatu Makame
MKUU wa kitengo cha mazao ya biashara kutoka Idara ya Misitu na Maliasili Zisizorejesheka, Is-haka Mohamed Abdulwakil,
ametoa wito kwa wakulima wa karafuu kuwa na utamaduni wa kuitunza mikarafuu
baada ya mavuno.
Wito huo aliutoa ofisini kwake
Maruhubi,wakati akizungumza na mwanduishi wa habari hizi.
Alisema kumejitokeza mtindo wa
baadhi ya wakulima kutokuwa na utamaduni wa kuitunza mikarafuu baada ya mavuno na kusababisha mavuno ya karafuu kupungua
msimu hadi msimu.
Alisema serekali inatumia
gharama kubwa kuendeleza zao la karafuu, hivyo ni wajibu wa wakulima
kuhakikisha wakati wote mikarafuu inakuwa safi.
Aidha aliwahimiza wakulima
wapya wa mikarafuu kuomba kupatiwa miche ya mikarafuu ambayo hutolewa bure ili
kuhakikisha kilimo cha mikarafuu kinarejea katika asili yake.
Alisema kutokana umuhimu wa zao
hilo wameandaa mafunzo maalum yatakayowasaidia wakulima kujua namna ya
kuitunza
na kuihifadhi mikarafuu.
Nae Ofisa wa uzalishaji miche
kutoka idara hiyo, Rashid Nasor Rashid, alisema mikakati yao ni kuhakikisha kila mwaka wanazalisha miechi
milioni moja na kuigawa kwa wakulima.
No comments:
Post a Comment