Na Kauthar Abdalla
JUMUIYA ya maradhi
yasiyoambukiza Zanzibar, inakusudia
kufanya uchunguzi wa awali wa kansa ya shingo ya kizazi kwa wanawake walio na
umri wa miaka 35 na kuendelea.
Akizungumza na waandishi wa
habari ofisini kwake Mpendae, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Ali Mansour Vuai,
alisema wanawake wengi wanaathiriwa na ugonjwa huo kutokana na dalili zake
kutojitokeza mapema.
Alisema kuna jumuiya mbali mbali zinazoshughulikia
maradhi yasiyoambukiza kama presha na kisukari
lakini hakuna jumuiya ambayo inashughulika na saratani ya shingo ya
kizazi kwa sababu ni maradhi ambayo yana usiri mkubwa kwa wanawake.
Alisema ugonjwa huo una hatari
kubwa ya kuwapotezea maisha wanawake kwani unahitaji uchunguzi wa kina na una gharimu
fedha nyingi kutibiwa.
Pia alisema jumuiya hiyo inafanya kazi ya kitaifa lakini
inahitaji msaada wa kijamii ili ili ifanikiwe malengo yake.
Aliiomba jamii kuunga mkono
utafiti huo pamoja na kuisaidia jumuiya kufikia malengo yake.
No comments:
Post a Comment