Habari za Punde

Mwakilishi Kikwajuni asaidia Saccos ya wanawake

Na Zainab Anuwar
 
MWAKILISHI wa jimbo la Kikwajuni, Mahamoud Mohamed Mussa, amewataka akina mama wa Saccoss ya Ishara Njema, kuendelea kuimarisha umoja na ushirikiano ili waweze kujiletea maendeleo.

Aliyasema hayo Kilimani  wilaya ya mjini Unguja, wakati akiwa katika ziara ya kukitembelea Saccoss hiyo kwa lengo la kujua maemdeleo pamoja na changamoto zinazowakabili wanachama.

Alisema ni vyema akina mama hao kukiendeleza kwa ufanisi zaidi kikundi chao ili kiweze kuwasaidia katika mfumo mzima wa maisha na kuachana na tegemezi.

Mwakilishi huyo alisaidia shilingi 300,000 ili kusaidia maendeleo ya kikundi hicho.

Katibu wa Saccoss hiyo, Rukia Omar , alisema lengo la  kikundi hicho ni kuwajengea uwezo akina mama kujiajiri na kupunguza utegemezi.

Hata hivyo, alisema wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwmeo  kutokuwa na soko la uhakika la kuuzia bidhaa zao.


Nae Mwenyekiti wa Saccoss hiyo, Hidaya Abdalah, alisema kutokuwa na mtaji wa kutosha ndio changamoto ya msingi katika Saccoss hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.