PAMOJA na makumbusho haya ya msikiti wa wahindi jamii
ya mabohora, uliopo kijiji cha Jambangome wilaya ya Mkoani Pemba, kusemekana
kama ndio eneo la mwanzo kuhamiwa kisiwani Pemba tokea karne ya 18 hadi ya 20,
bado serikali kupitia Idara yake ya makumbusho hawajaona umuhimu wa
kuyahiafadhi na kusababisa kuzongwa na pori na kupoteza fedha za kigeni
MKUU wa kamisheni ya utalii Pemba mwalimu Suleima
Amour, akizungumza na waandishi wa habari kwenye eneo lenye makumbusho ya
waanzilishi wa kisiwa cha Pemba, wahindi jamii ya mabohora kwenye karne ya 18
hadi 20, kijiji cha Jambangome wilaya ya Mkoani Pemba, ambapo kamisheni ya
utalii inaendelea na kampeni yake ya utalii kwa wote
ENEO la Tandauwa wilaya ya Chakechake Pemba, ambapo
panasemekana palikuwa na kisima cha utafiti wa mafuta kwenye miaka ya 1961,
kazi iliofanywa na kampuni ya BP Schell, ambapo kwa sasa limebakia bila ya
kuhifadhiwa
GATI iliko kijiji cha bahari ya Tundauwa wilaya ya
Chakechake Pemba, ambayo kwenye miaka ya 1960 hadi mwaka 1962 ilikuwa ikitumiwa
na kampuni ya BP Schell kwa ajili ya kushushia vifaa na magari yao wakati
walipokuwa wakiendesha utafiti wa mafuta kisiwani humo, ambapo kwa sasa gati
hiyo inayoweza kuingizwa kwenye makumbusho ya taifa imetelekezwa.
KATIKATI Mkuu wa Kamisheni ya utalii Pemba
mwalimu Suleiman Amour akiwa na mzee Mohamed Bakari Juma (71) ambae alikuwa akiutembeza
ujumbe wa waandishi wa habari na watendaji wa kamisheni ya utalii, ili kutoa
historia halisi ya kujengwa kwa gati hiyo kwenye miaka 1960 ili kampuni ya BP
Schell kupitishia vifaa wakati ikifanya utafiti wa uchimbaji mafuta kijiji cha
Tundauwa Pemba.
KATIBU wa ‘’Wawi spice farm’ Ali Mohamed Ibrahim
akizungumza na waandishi wa habari, juu ya malengo ya kuanzisha kituo cha
utalii wa ndani, wakati waandishi hao walioambatana na watendaji wa kamisheni
ya Utalii, walipofika eneo hilo ikiwa ni sehemu ya kutangaaza utalii kwa wote.
MWENYEKITI ushirika wa ufugaji samaki ‘Sir
Fish Firm’ uliopo Pujini kibaridi aliembele Ahmed Salim Issa,
akiuongoza ujumbe wa waandishi wa habari na watendaji wa kamisheni ya utalii
Pemba, ili kuangalia ufugaji wa samaki, ikiwa ni ziara maalumu ya kuimarisha
sera ya utalii kwa wote.(Picha na Haji Nassor Pemba)
Habari nzuri ila jina la kampuni nadhani ni Shell na sio Schell
ReplyDelete