Pamoja jukumu kubwa la mkutano wa kamati ya maandalizi, Mhe. Spika alipata nafasi ya kufika katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa ambapo alipokelewa na Naibu Mwakilishi wa Kudumu Balozi, Ramadhani Mwinyi. Hapa Mhe. Spika akisaini kitabu cha wageni na pembeni yake ni Balozi Ramadhan Mwinyi na aliyeketi ni Bw. Eliufoo Ukhotya kutoka Ofisi ya Spika
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akizungumza na wajumbe wa kamati ya maandalizi ya Mkutano wa Nne wa Dunia wa Maspika wa Mabunge, wajumbe wa kamati hiyo akiwamo Mhe, Spika Anne Makinda ( Mb) walikutana kwa siku mbili hapa Umoja wa Mataifa
Hapa ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Jan Eliasson akisalimiana na Mhe. Anne Makinda ( Mb) Spika wa Bunge Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Na
Mwandishi Maalum, New York
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, amesema, kutokana na dunia kukabiliwa na matatizo mengi na ambayo yanatokea kwa wakati mmoja.Kuanzia mlipuko wa
Ebola, vita na machafuko , ugadi, uhalifu wa kupangwa na mabadiliko ya tabia nchi. Hakuna nchi ambayo inaweza kujidai
kwamba inaweza kusimama peke yake.
Ameyasema hayo siku ya jumanne wakati
alipokuwa akibadilishana mawazo na wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano
wa Nne wa Dunia wa Maspika wa Mabunge,
mkutano utakaofanyika mwezi Agosti, 2015
Jijini New York.
Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda ( Mb) ni kati ya wajumbe wa
Kamati hiyo ya Maandalizi ambayo imekutana kwa siku mbili hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Ban Ki Moon, amewaambia Maspika
hao kwamba, dunia hivi sasa inakabiliwa
na matatizo mengi sana na kuwa baadhi yake
yanasababishwa kwa viongozi
kutosikiliza sauti za wananchi wao.
“ kuna matatizo mengi yanayotokea na
mengine yanatokea kwa sababu viongozi hawasikilizi sauti za wananchi wao.
Kuna pengo kubwa kati ya wananchi na viongozi wao”. amesema Katibu Mkuu.
Na kwa sababu hiyo amesema, maspika
wa mabunge na wabunge wao wanayonafasi kubwa ya kuepusha baadhi ya matatizo kwa
kufikisha sauti na wananchi waliowachagua kwa viongozi wao.
Amesema bila ya ushirikiano ndani ya taifa kama nchi moja
moja na katika ngazi ya kimataifa hakuna nchi ambayo inaweza kuhimili changamoto zinazotokana na matatizo ya aina yoyote ile.
“ Hakuna nchi inayoweza kusimama peke
yake, wote lazima tushirikiane na kuwa
kitu kimoja, lazima sote tuonyesha
utashi wa kisiasa, tusaidiane kwa
raslimali tulizonazo, tufanya kazi kwa pamoja
ili kuyashaghulikia matatizo tuliyonayo” amesema Ban Ki Moon.
Akatoa mfano wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola kama moja ya
tatizo kubwa ambalo siyo tu limeleta madhara makubwa bali pia athari zake zimeleta mtikisiko mkubwa katika
sekta nzima ya afya.
Amesema kutokana kasi ya
kusambaa kwa ugonjwa huo na athari zake
kiuchumi, kijamii na kimaendeleo ni wazi kwamba, pasipo kuwa na nguvu ya
pamoja, ushirikiano thabiti wa raslimali tulizo nazo hakuna nchi iwe kubwa
kiasi gani au ndogo inayoweza kujihakikisha usalama dhidi ya ugonjwa huo.
Akizungumzia nafasi ya Maspika na
Mabunge wanayoyaongoza katika
kukabiliana na matatizo yanayoikabili dunia hivi sasa iwe katika ngazi ya nchi husika au katika ngazi ya kimataifa.
Ban Ki Moon alikuwa na haya ya kusema.
“ Nyinyi mnawakilisha wananchi
waliowachagua, mnawakilisha sauti zao,
ninayoheshima kubwa sana kwenu pamoja na
kazi mnazozifanya”
Akawachekesha maspika hao kwa kusema, katika maisha yake
yote ya utumishi hajawahi kufikilia kuwa mbunge ingawa amekuwa na uhusiano mzuri
na wanasiasa.
Amesema pamoja
na kuwa wawakilishi wa wananchi, wabunge ndio wanaopitisha bajeti za
serikali zao ikiwa ni pamoja na
kupitisha mikataba ya kimataifa.
Na hivyo amewataka wabunge hao kushirikiana kwa
karibu na serikali zao na hasa katika kupindi
kijacho ambacho serikali zitakuwa
zikijianda na utekelezaji wa ajenda na
malengo mapya ya maendeleo endelevu baada ya 2015.
“ Hata kama serikali zitakuwa na mipango mizuri , kama bunge
halitapitisha bajeti inayotakiwa ni wazi
kwamba mipango hiyo haitaweza kutekelezwa kwa ukamilifu, kwa hiyo moja ya rai yangu
kwenu shirikianeni na serikali ili muweze kuwaletea
wananchi wenu maendeleo endelevu” amesisitiza Katibu Mkuu.
Katika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw Jan
Eliasson akibadilishana mawazo na
wajumbe wa kamati hiyo ya
Maandalizi amesema hakuna mtu anayeweza
kufanya kila kitu lakini kila mtu
anaweza kufanya jambo fulani.
Naibu
Katibu Mkuu katika mazugumzo
yake pamoja na mambo mengine ametilia sana mkazo
umuhimu wa amani, usalama,
utawala wa sheria na demokrasia kama
baadhi ya nguzo za maendeleo.
Akasema yapo
mambo muhimu ambayo mwananchi wa
kawaida anayataka ambayo ni amani, maendeleo,
serikali na taasisi anazoziamini, ushiriki na sauti yake kusikika katika
mambo yenye maslahi kwake.
“ Wananchi wanatuangalia sisi
viongozi wao, je tunawashuri ipasavyo,
je tunazingatia maslahi yao. Wananchi
wa leo siyo wale wazamani, wanauelewa na ufahamu mkubwa wa mambo yanayowazunguka na teknolojia ya mawasiliano
imewaongezea uelewa huo. Wanajua
nini wanachokitaka na nini wanakitarajia
kutoka kwa viongozi wao” amesisitiza Naibu Katibu Mkuu.
Amewataka Maspika, wabunge pamoja na mihimili mingine ya dola kuwa
na mtizamo mpya na fikra mpya na pana zaidi za siyo tu
kushughulikia matatizo ya wananchi wao lakini pamoja na matatizo mbalimbali
yanayoikabili dunia hivi sasa.
Na kuongeza kuwa kila mtu katika
nafasi yake iwe serikali, bungeni, katika sekta binafsi au katika asasi zisizo
za kiserikali anaowajibu anaotakiwa kuutekeleza.
Na kwamba makundi hayo na mengine mengi ya kijamii kwa umoja wao yanatakiwa kuingia
katika kipindi kipya cha ushirikiano na
mshikamano.
No comments:
Post a Comment