TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
01 Nov 2014
Ndugu waandishi wa habari ,
Kwanza napenda kumshukuru M/Mungu kwa
mapenzi yake ya kutukutanisha hapa leo tukiwa wazima wa afya , pili napenda
kuchukua fursa hii kukushukuruni nyie waandishi wa habari kwa kupoteza muda
wenu na kuja kushirikiana na sisi , kwa hili tunawashukuru sana.
Ndugu waandishi wa habari,
Tuliopombele yenu ni viongozi halali
wa shirikisho la wanafunzi wa elimu ya juu Tanzania (TAHLISO) ambao
tumechaguliwa kihalali tarehe 14/12/2014 kufuatia uchaguzi mkuu wa TAHLISO
uliofanyika chuo cha Afya Bugando Mwanza, ambapo uchaguzi huo ulimchagua ndugu
Mussa Mdede (Mwenyekiti), ndugu Abdi Mahamoud Abdi (Makamo mwenyekiti), ndugu
Halima Bakari Nyange (katibu mkuu), ndugu Rajab Ali Rajab (Naibu katibu mkuu),
ndugu Mollel Hillary (Mhazini) na ndugu Khamis Hamza Khamis (Mhazini Msaidizi).
Ndugu waandishi wa habari
Kwa mujibu wa katiba ya shirikisho la
vyuo vikuu Tanzania (TAHLISO) ibara ya 5 (2) NI MARUFUKU kwa kiongozi yeyote haswa wa ngazi ya juu katika
TAHLISO kushiriki katika shuhuli zozote za kisiasa haswa kupanda juu ya
majukwaa ya kisiasa kwani kufanya hivyo nikuiwakilisha taasisi katika siasa wakati
TAHLISO ni taasisi ya kijamii, lakini Mh. Mwenyekiti wa shirikisho la wanafunzi
wa Elimu ya juu Tanzania (TAHLISO) ndugu Mussa Mdede alishiriki katika vugu
vugu la siasa za vyama vingi kwa kugombea Ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo
la kalenga kufuatia kifo cha aliekua Mbunge wa jimbo hilo Mh. Marehemu Mgimwa
Ndugu waandishi wa habari,
Kwa kua katiba ya TAHLISO hairuhusu
viongozi kujiingiza kwenye mambo ya kisiasa tarehe 3 April 2014 katika chuo cha
kodi jijini Dar es salaam.TAHLISO tulikutana katika kikao cha senate na kikao kiliamua kumuondoa
madarakani ndugu Mussa Mdede kutokana na kuenda kinyume na katiba hiyo pia
kikao kiliamua nafasi yake ikaimiwe na makamo mwenyekiti Ndudu ABDI MAHAMOUD
ABDI mpaka pale Shirikisho litakapofanya uchaguzi mwengine au ikionekana kuna
haja ya kufanya uchaguzi mdogo kabla ya uchaguzi wa December mwaka huu. Kwa
kushangaza mara tu baada ya miezi sita kupita na kubadilika kwa viongozi katika
serikali za wanafunzi katika vyuo mbali mbali Ndugu Mussa Mdede aliitisha kikao
na kuwadanganya viongozi wapya wachache waliofika katika kikao hicho na kuendelea
kujitangaza kwamba yeye ni mwenyekiti wa TAHLISO katika vyombo mbalimbali vya
habari ikiwemo tv na magazeti pamoja kuwashawishi wanafunzi wa vyuo vikuu
kuandamana na kufanya migomo kwa ajili ya kuikomoa serikali.
Ndugu waandishi wa habari,
Hapa ndo tunataka mtutegee masikio
yenu, vipaza sauti vyenu pamoja na kamera zenu kua Shirikisho la vyuo vikuu
Tanzania TAHLISO na Shirikisho la vyuo vikuu Zanzibar ZAHILFE tunakemea vikali
tabia ya baadhi ya viongozi wa siasa nchini kuanzisha tabia mbaya ya kuwaita
wanafunzi wa vyuo vikuu kisiri siri katika majumba yao, mahoteli mbalimbali na
kupanga nao vikao vya siri, kualika viongozi wengi wa serikali za wanafunzi
kutoka Tanzania bara kuja kushiriki mikutano mikubwa katika hoteli zilizopo
Zanzibar ili kuweza kuwataka wanafunzi
wa vyuo vikuu kuwaunga mkono katika maadhimio yao. Shirikisho la vyuo vikuu
nchini tunawaomba wanasiasa kuwacha tabia hiyo mara moja kwani tabia hiyo ndio
iliyopelekea machafuko katika nchi mbali mbali duniani kama vile Libya,
Bakhrein, Misri,Uturuki na nchi nyengine nyingi kuwataka wanafunzi kuandamana
na kuwaahidi mambo mengi makubwa ambayo kiuhalisia hayatekelezeki na kuingiza
nchi katika vita visivyo koma kama tunavyoona katika nchi kama vile LIBYA na
MISRI katika kipindi hiki
Vile vile tunaziomba serikali zote mbili ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia vyombo husika pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kulifuatilia suala hili na kulikataza mara moja kutokana na sababu kwamba amani ya nchi ikiondoka ni vigumu sana kuirudisha vile vile mambo haya yanaweza kuligharimu taifa kwa kupoteza wananchi wengi wasiokua na hatia.
Ndugu waandishi wa habari
MWISHO tunanapenda kuchukua fursa hii
kuwaomba wanafunzi wote wa Tanzania kuitafuta katiba pendekezwa kuipitia na
kuisoma katiba pendekezwa ya bunge maalum sura kwa sura ibara kwa ibara na neno
kwa neno, ili kuifahamu na kuielewa na kuwacha kuwasikiliza wanasiasa ambao
wanamalengo yao binafsi na ikifika april mwakani kuja kuipigia kura katiba hii
kwa kua tulishirikishwa tokea mwanzo kwenye kutoa maoni ya mtu mmoja mmoja,
vikundi, mabaraza na mwisho kushirikishwa katika hatua muhimu ya bunge maalum la katiba ambapo wanafunzi
wa vyuo vikuu kupitia taasisi zetu hizi ya ZAHILFE na TAHLISO tulitoa wawakilishi
na kufaanikiwa kuingiza maoni yetu katika katiba na kueka historia ya taifa na
kushiriki kuandaa misingi mizuri ya nchi yetu hususan katika vipengele vyote
vinavyo ashiria kuufanya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kua imara zaidi kwa
kuziondoa kero zote za muungano huu uliodumu kwa muda wa miaka 50 sasa.
Imetolewa na:
Abdi Mahamoud Abdi
Makamo mwenyekiti
TAHLISO
Du! hii kali mumechaguliwa kabla ya tarehe kufika nyie kweli viongozi wajao, kwa speed hio maendeleo yatakuja tu
ReplyDelete