Habari za Punde

Wakulima 7 Wakabidhiwa Matrekta leo

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akikabidhi funguo za trekta kwa Mwalimu wa Shule ya msingi Kwadelo Bw. Hamza Haji, matrekta saba yalikabidhiwa leo kwa wakulima chini ya usimamizi wa Diwani wa Kwadelo Alhaji Omari Kariati
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akikabidhi funguo za trekta kwa Dk. Edmund Mndolwa ambaye ni Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa ikiwa sehemu ya matrekta saba yaliotolewa na Alhaji Omari Kariati Diwani wa Kwadelo.                                                   
Moja ya matrekta waliokabidhiwa wakulima ,Alhaji Omari Kariati ameshatoa matrekta 100 mpaka leo tarehe 5 februari 2015.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi matrekta saba kwa wakulima yaliyotolewa na Diwani wa Kwadelo Alhaji Omari Kariati ambapo aliwataka viongozi kushiriki shughuli za wananchi.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akijaribu kuendesha trekta mojawapo kati ya matrekta saba aliyokabidhi funguo kwa wakulima kutoka sehemu mbali mbali nchini, waliopanda trekta hilo kushoto ni Mjumbe wa NEC kutoka Wilaya ya Korogwe Vijijini Dk. Edmund Mndolwa na kulia ni Diwani wa Kwadelo Alhaji Omari Kariati.
Mafundi wakiendelea kuunganisha matrekta ya Kariati ambayo yametolewa na Alhaji Omari Kariati.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi ya Kariati inayoshughulika na matrekta ya kilimo Kinondoni Vijana Jijini Dar es salaam.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na MNEC wa Korogwe Vijijini Dk. Edmund Mndolwa (kushoto) kulia ni Diwani wa Kwadelo Alhaji Omari Kariati kwenye ofisi ya Kariati inayoshughulika na matrekta ya kilimo Kinondoni Vijana Jijini Dar es salaam.(Picha na Adam Mzee)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.