Habari za Punde

Maalim Seif afutari pamoja na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akisalimiana na Rais wa serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu Ust. Ali Abdallah, alipowasili chuoni hapo kwa ajili ya kufutari na wanafunzi wa chuo hicho.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na wanafunzi wa Chuo kikuu cha Zanzibar Tunguu, baada ya kufutari na wanafunzi hao.
 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dkt. Idrissa Muslih Hijja, akitoa nasaha kwa wanafunzi hao kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi.
 Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Othman Ngwali, akizungumza katika hafla hiyo baada ya futari iliandaliwa na wanafunzi wa Chuo Kukuu cha Zanzibar (ZU), Tunguu.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akijumuika na viongozi wa Mkoa wa Kusini Unguja, masheikh na wanafunzi wa ZU katika futari. Kutoka kulia ni Naibu Kadhi Mkuu Sheikh Othman Ngwali, Rais wa serikali ya wanafunzi (ZU) ust. Ali Abdalla na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dkt. Idrisaa Muslih Hijja.
 Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU), wakijumuika katika futari waliyomualika Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad. (Picha na Salmin Said, OMKR)

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU), wakijumuika katika futari waliyomualika Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad. (Picha na Salmin Said, OMKR)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.