Habari za Punde

WAZAZI MKOA WA MAGHARIBI WAFANYA KONGAMANO KUELEKEA WIKI YA WAZAZI

Mkuu wa Oganaizesheni Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Omar Ibrahim Kilupi akifunguwa kongamano la jumuiya ya wazazi wa Mkoa wa Magharibi Kichama,  lililofanyika skuli ya Ali Hassan Mwinyi Bububu Wilaya ya Magharibi A.

Na Fauzia Mussa Maelezo.05.05.2024.

Mkuu wa Oganaizesheni Afisi Kuu ya chama cha mapinduzi 

Zanzibar Omar Ibrahim Kilupi amezitaka jumuiya za chama 

cha Mapinduzi kuweka mikakati ya kuwatambua vijana ambao hawajasaliliwa katika datfari la wapiga kura ili waweze 

kusajiliwa.


Akifungua kongamano la jumuiya ya wazazi wa Mkoa wa 

Magharibi Kichama huko Skuli ya Ali Hassan Mwinyi Bububu 

amesema kuna baadhi ya vijana hawakujiandikisha katika 

awamu iliopita hivyo ni vyema kuwatambua na 

kuwahamasisha kujiandikisha katika awamu ijayo.


Amezitaja baadhi ya sababu zilizopelekea vijana hao 

kutojisajili kuwa ni pamoja na kutotimiza umri wa miaka 18 

pamoja na kuwa mbali na vituo vya kujiandisha kwa kipindi 

hicho.


Aidha amezitaka jumuiya hizo, kuhakikisha vijana wote 

waliotimiza vigenzo wanajisajili ili kuweza kupata vijana 

wengi watakaoendelea kukiweka madarakani chama cha 

Mapinduzi ifikapo 2025.


“Kuna kundi la wananchi ambao wana sifa za kujisajili lakini 

hawajaenda kujisajili na kama tunavyojuwa kama hukujisajili 

katika daftari la kudumu la wapiga kura hutoweza kupiga 

kura,tuendeni tukahamasishe ili tusije kumuacha mtu 

nyuma.” alisema Kilupi.


Aidha amesema lengo la mafunzo hayo ni kutoa elimu ya 

uchaguzi na mmongonyoko wa maadili na kuwataka 

kuyafanyia kazi mafunzo walipopewa sambamba na kuwa 

mabalozi wazuri kwa wenzao.


Kwa upande wake Mlezi wa Mkoa wa magharibi kichama 

ambae pia Mwakilishi wa viti maalum kupitia jumuiya ya 

wazazi mkoa wa kusini Unguja Mhe. Sabiha Filfil Thani 

amesema kuna kila sababu ya Dkt. Hussein Ali Mwinyi 

kuendelea kubaki madarakani katika Uchaguzi unaotarajiwa 

kufanyika hapo mwakani kutokana na kutekeleza kwa vitendo 

ilani ya chama hicho.


“Ilani ya CCM ilimtaka rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa 

Baraza la Mapinduzi kujenga madarasa 1,500 kwa Skuli za 

Unguja na Pemba ambapo amevunja rikodi kwa kujenga 

madarasa 2273 sawa na silimia 150 ya malengo ya ilani ya 

chama cha Mapinduzi.” amefahamisha Mlezi huyo.


Katika kongamano hilo mada mbili ziliwasilishwa na 

kujadiliwa ikiwemo mmongonyoko wa maadili na uchaguzi 

Mkuu ambapo Kauli mbiu ni ”USHINDI WA CCM 2024-

2025   JUMUIYA YA WAZAZI TUPO MSTARI WA MBELE”.

Mlezi wa Mkoa wa magharibi kichama ambae pia Mwakilishi wa viti maalum kupitia jumuiya ya wazazi mkoa wa kusini Unguja Mhe. Sabiha Filfil Thani akizungumza katika kongamano la jumuiya ya wazazi Mkoa wa Magharibi Kichama huko Skuli ya Ali Hassan Mwinyi Bububu Mkoa wa Mjini Magharibi.


Vijana wa Sanaa wa kikundi cha Toto boy  Hawai  Ibrahim Juma Shaaban na Hamad Seif Mohammed wakitoa burudani yenye maadhui ya athari za mmong'nyoko wa maadili katika Kongamano la jumuiya ya wazazi, lililofanyika Skuli ya Ali Hassan Mwinyi Bububu Unguja.

PICHA NA FAUZIA MUSSA- MAEEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.