Habari za Punde

WanaCCM mkoa wa Kusini Unguja kuendelea kumuunga mkono Dk Shein


  
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar                                  13.10.2015
---
WANANCHI na WanaCCM wa Mkoa wa Kusini Unguja wamepongeza juhudi zilizochukuliwa na Dk. Shein katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ikiwa ni pamoja na kuwasogezea huduma za maji kwa asilimia 80 katika Jimbo la Chwaka huku wakimuhakikishia kiongozi huyo kuendelea kumuunga mkono.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano wa Kampeni ya uchaguzi wa CCM uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi na wanaCCM uliofanyika uwanja wa  mpira Chwaka, Jimbo la Chwaka, Wilaya ya Kati Unguja, Mkoa wa Kusini Unguja, viongozi wa CCM waliohudhuria mkutano huo kwa nyakati tofauti walisema kuna CCM ndio chama pekee kinachojali maslahi wa wananchi.

Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kati Hassan Mrisho Vuai alimpongeza Dk. Shein kwa kutekeleza vyema Ilani ya Uchaguzi ya CCM, walieleza kuwa Dk. Shein ameweza akutekeleza kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi sambamba na kuongoza vyema Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Alieleza kuwa sekta mbali mbali za maendeleo zimeimarika ikiwemo sekta ya maji ambayo imeimarika kwa asilimi 80 ambapo tatizo la maji katika Jimbo la Chwaka limepungua kwa kiasi kikubwa.

Aidha, kiongozi huyo alieleza kuwa CCM ndicho chama kilicholeta ukombozi, misingi ya kutela umoja, amani na maendeleo kwa Watanzania na hawana sababu ya kuacha kukiunga mkono chama hicho kwani wazee wao wamewaachia chama hicho na wataendelea kukiunga mkono daima.


Alieleza kuwa upinzani si ubabe, na kuwataka wafuasi wa chama cha CUF wanapokwenda katika Mikoa yao waweke heshima na kusema haifai kuanza kutoa matusi hasa pale wanapowaona wanachama wa CCM, na kusema kuwa wao wanafuata sheria na taratibu za Tume na kuwaomba wanapokwenda katika maeneo yao wajue kuwa  kuna watu na heshima zao na kusisitiza kuwa 'kuku hafundishwi kutaga.

Aidha, viongozi wa CCM Mkoa huo wa Kusini Unguja walimpongeza na kumueleza kuwa Kusini watatoa kura za ndio siku ya tarehe 25 kwa viongozi wote wa CCM.

Viongozi wa chama wa Mkoa huo walieleza kuwa wanachama wa CCM hawataki shari wala ugomvi licha ya dalili mbali mbali za shairi na ugomvi zinazooneshwa na wafusi wa vyama vya upinzani dhidi yao kikiwemo chama vha CUF.

Nae Modelin Kastiko alieleza mafanikio yaliopatikana katika Jimbo la Chwaka na kueleza bahati kubwa waliyoipata wanachakwa kwa kujengewa Chuo cha Maendeleo ya Fedha katika kijiji hicho.

Nae Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambaye pia, ni Waziri Kiongiozi mstaafu Shamsi Vuai Nahodha, aliwaeleza wanaCCM kuwa wana kazi kubwa ya kulinda Mapinduzi na kuulinda Muungano kwani anaamini kuwa maadui wa Mapinduzi na Muungano bado wapo.

Alisema kuwa mwaka 1995 kuna kiongozi mmoja wa CUF wakati wakihitimisha Kampeni za chama hicho alisema kuwa siku hiyo ndio mwisho wa Serikali inayoongozwa na mtu mweusi, na kusema kuwa wakipata Serikali watayaondosha Mapinduzi kwani hayana maana na yamepitwa na wakati.

Hivyo aliwaeleza wananchi wanaoyataka Mapinduzi na wanaoujali na kuupenda Muungano ni lazima  wamchague Dk. Shein, kwani ana historia ya kuupenda Muungano wa Serikali mbili, kuyapenda Mapinduzi, na anawahemshimu waaasisi wa Mungano na Mapinduzi hivyo kuna kila sababu ya kumchague Dk. Shein.

Alisisitiza kuwa hakuna kazi ngumu ya kuongoza Serikali ya Umoja wa Kitaifa kama ilivyo hivi sasa kwani kuna viongozi wanaowadanganya wananchi na kusema uongozo huku akisema kuwa kazi ya kuongoza Serikali hiyo ni lazima apatikane mtu mwenye sifa kama Dk. Shein.

Kutokana na hilo aliwaomba wananchi na wanaCCM kumchagua Dk. Shein na kusema kuwa iwapo wakimchagua watakuwa wanaunga mkono Sera za uhakika na zinazotekelezeka.

Alisema kuwa kama anatafutwa rais wa kuleta maendeleo basi Dk. Shein anatosha.

Waziri wa Maji, Ardhi na Nishati ambaye pia, ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Ramadhan Abdalla Shaaban nae aliendelea kulielezea suala la mafuta na kuwasisitiza wananchi kutodanganyika juu ya suala hilo kuwatokana na maelezo ya viongozi wa kambi ya upinzani.

Waziri Shaaban alisema kuwa mgombea urais kupitia chama cha CUF  Maalim Seif Sharif Hamad hivi karibuni alieleza kuwa Katiba inayopendekezwa haikutoa fursa ya kuchimba mafuta, na kutumia fursa hiyo kuisoma Katiba inayopendekezwa na mambo yanayohusu mambo ya Muungano ambapo suala la mafuta halipo.

Alieleza kuwa Kifungu cha 26 cha Katiba hiyo inayopendekezwa kimeelezea vizuri suala hilo na kusisitiza kuwa Sheria zote za mafuta zitatungwa na Baraza la Wawakilishi kwa mujibu wa Katiba inayopendekezwa huku akieleza kuwa suala la mafuta linashughulikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisema kuwa hakuna haja ya kupewa kura za ndio viongozi ambao wamekuwa wakiwadanganya wananchi na kuwataka wananchi wasidanganyike huku akisisitiza kuwa mafuta ya Zanzibar yatachimbwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na hivi sasa mchakato unaendelea.

Nae Waziri wa Kilimo na Maliasili Dk. Sira Ubwa Mwamboya alisikitishwa na baadhi ya madaktari ambao wamekuwa wakifanya mradi wa kuwatolesha fedha wananchi wakati tayari Dk. Shein ameshatangazia kuwa matibabu kwa wazazi hivi sasa yanatolewa bure.

Alisema kuwa miongoni mwa Madaktari hao ni Dk. Mwana ambae hivi sasa amekuwa akisimama kwenye majukwaa ya mikutano ya siasa kupitia chama cha CUF na kusema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haikufanya kitu kwenye Wizara hiyo wakati yeye mwenyewe alikuwa akifanya kazi hospitalini hapo na kufanya biashara za vifaa vya uzazi hospitalini hapo sambamba na kuwatolesha fedha wazazi wanaofika hospitalini hapo kujifungua kinyume na sheria za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Nae Balozi Ali Karume, alisema kuwa anaamini kuwa Dk. Shein atamalizia vizuri kazi ambazo ameshaanza kuzifanya, hivyo ana kila sababu ya kuchaguliwa tena kuiongoza Zanzibar.

Alisema kuwa Dk. Shein ana sifa zote za kuendelea kuwa Rais wa Zanzibar na kusisitiza kuwa hakuna maendeleo makubwa kama kuishi katika nchi yenye amani na utulivu kama ilivyo Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Shein.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.