Habari za Punde

CAF Yatowa Semina kwa Viongozi wa Vilabu Zanzibar Kujiendesha Kukuza Soka katika Vilabu Vyao.

 
Mjumbe wa Kamati wa Muda ya ZFA Hashim Salum akitowa maelezo kabla ya kuanza kwa Semina hiyo kwa Viongozi wa Vilabu vya Mchezo wa Mpira Zanzibar ulioandaliwa na CAF kwa Kushirikiana na ZFA iliofanyika katika Ukumbi wa Bahari Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar na kuwashirikisha Viongozi wa Vilabu vya Daraja la Kwanza Zanzibar. 
Mwenyekiti w Kamadi ya Muda ya ZFA Hussein akizungumza wakati wa Semina hiyo ya Viongozi wa Michezo Zanzibar kuwajengea Uwezo wa kuongozi vilabu vyao kujitegemea ilioandaliwa na CAF kwa kushirikiana na ZFA iliofanyika katika Ukumbi wa Bahari Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar. 
Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Zanzibar BMZ Mwalim Khamis Ali, akiwahutubia na kufungua Semina ya Siku mbili ya Viongozi wa Michezo Zanzibar ilioandaliwa na CAF kwa kushirikiana na ZFA iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar. 
Wakufunzi wa Shirikisho la Mpira Barani Afrika CAF, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa BMZ Mwalim Khamis Ali akifungua Mafunzo hayio ya Siku mbili kwa Viongozi wa Vilabu vya Michezo Zanzibar

Mkufunzi kutoka Shirikisho la Mpira Barani Afrika CAF George Kasengele, kutoka Zambia akitowa Mada wakati wa Semina hiyo kwa Viongozi wa Vilabu vya Mpira Zanzibar. jinsi ya kujiendesha katika shughuli zake za michezo katika vilabu vyao.  

Waandishi wa habari za Michezo Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa mkutano wakifuatilia Madac zinazowakilishwa na Wakufunzi wa CAF kwa Viongozi wa Vilabu Zanzibar. 
Waandishi wa habari za Michezo Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa mkutano wakifuatilia Madac zinazowakilishwa na Wakufunzi wa CAF kwa Viongozi wa Vilabu Zanzibar.






No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.