Habari za Punde

"YAVUNA" MAMIA YA WANACHUO WA UDSM NA TUMAINI KAMPASI YA DAR ES SALAAM, WAJIUNGA NA MPANGO WA PSS, VANESSA MDEE, JOYCE KIRIA NAO NDANI



Mwanamuziki nyota nchini Vanes Mdee, akiweka dole gumba tayari kuchapa kwenye fomu ya kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF wakati wa kongamano lililowakusanya wanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Shule ya Biashara na kufanyika chuoni hapo mwishoni mwa wiki. Mamia ya wanachuo walijiunga na mpango huo baada ya kupata elimu ya faida za kujiunga na mpango huo. Wanaoshuhudia, kutoka kulia ni Balozi wa PSPF, Flaviana Matata ambaye ni mwanamitindo wa kimataifa anayefanya kazi zake Ulaya na Marekani, Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, PSS wa Mfuko huo, Mwanjaa Sembe, na Afisa Masoko na Uhusiano wa PSPF, Rahma Ngassa.



Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mwanjaa Sembe, (aliyesimama), akizungumza kwenye kongamano la wanafunzi wanawake wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (Shule ya Biashara), chuoni hapo. Kushoto ni Balozi wa PSPF, Mwanamitindo wa Kimataifa anayefanya kazi zake Ulaya na Marekani, Flaviana Matata

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.