Habari za Punde

Hafla ya Kuapishwa Wajumbe Saba wa Baraza Walioteuliwa na Rais wa Zanzibar Dk Shein.


Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia Chama cha AFP Mhe Said Soud Said, akiwasili katika jengo la Baraza la Wawakilishi Zanzibar cha ajili ya kula kiapo baada ya kuteuliwa Nafasi hiyo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein.
Mwakilishi wa Nafasi ya Kuteuliwa na Rais wa Zanzibar Mhe Said Soud Said akisalimiana na Mwandishi wa Kituo cha TV cha Channel ten Ndg Munir Zakaria wakiwa katika jengo la Baraza la Wawakilishi Chukuwani Zanzibar.
Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Nafasi ya Kuteuliwa na Rais wa Zanzibar Juma Ali Khatib wa Chama cha ADA-TADEA akiwasili katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya kuapishwa kwa ajili ya kuaza kazi ya Kuwawakilishi Wananchi wa Zanzibar. 
Mhe Juma Ali Khatb wa Chama cha ADA -TADEA , akisalimiana na Mhe Balozi Amina Salum Ali wa Chama cha Mapinduzi wakati walipowasili katika viwanja vya Baraza la Wawakilishi kuhudhuria hafla ya kuapishwa kuwa Wajumbe wa Baraza baada ya kuteuliwa na Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein.















































No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.