Mkufunzi wa Mafunzo ya Ujasiriamali yanayoendeshwa na benki ya TIB katika viwanja vya Sabasaba, Louis Mkuku, akitoa mafunzo kwa baadhi ya wahudhuriaji wa semina hizo zinazoendelea katika viwanja vya Sabasaba.
Baadhi ya wafanyabiashara wakifatilia mafunzo ya uajasiriamali yanayoendeshwa na benki ya TIB katika viwanja Sabasaba.
Mkufunzi wa Mafunzo ya Ujasiriamali yanayoendeshwa na benki ya TIB katika viwanja vya Sabasaba, Louis Mkuku, akitoa mafunzo kwa baadhi ya wahudhuriaji wa semina hizo zinazoendelea katika viwanja vya Sabasaba.
Mkufunzi wa Mafunzo ya Ujasiriamali yanayoendeshwa na benki ya TIB katika viwanja vya Sabasaba, Louis Mkuku, akitoa mafunzo kwa baadhi ya wahudhuriaji wa semina hizo zinazoendelea katika viwanja vya Sabasaba.
Benki ya
TIB kwa kushirikiana na Taasisi ya Ujasiriamali na Uongozi wa Biashara (IMED) wanaendesha
mafunzo ya bure ya ujasiriamali katika banda la TIB lilipo katika viwanja vya
Sabasaba.
Mafunzo
hayo pia yanajumuisha elimu katika maeneo ya uongozi na sheria za biashara,
masoko, utawala wa fedha pamoja na utawala wa biashara yanalenga wajasiriamali
wadogo wadogo na wa kati ili kuwajengea uwezo wa kukuza biashara zao.
Akizungumzia
mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB, bwana Charles Singili,
alisema wameamua kutoa mafunzo hayo katika msimu huu wa Sabasaba ili kuwafikia
wafanyabiashara wengi zaidi pamoja na wananchi wa kawaida.
‘Mafunzo
haya ni bure, na yanafanyika katika banda letu la TIB hapa Sabasaba na wananchi
wote wanakaribishwa kuja kujifunza ili waweze kuendesha biashara zao kwa faida
na mafanikio’ alisema bwana Singili.
Mafunzo
hayo ambayo yamejikita katika kuwapa wafanyabiashara mbinu za kuendesha miradi
yao pamoja na kutumia vizuri mikopo inayotolewa na benki hiyo yanafanyika kuanzia
saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana, na yataendelea hadi tarehe 4 ya mwezi
Julai.
‘Kimsingi
mafunzo haya yanaendana na dhima ya mwaka huu ya maonyesho ya Sabasaba,
Kuunganisha Uzalishaji na Masoko, na
hivyo kwa elimu tutakayowapa wajasiriamali tunaamini wataweza kupanua wigo wa
masoko ya biashara zao’ alimaliza bwana Singili.
Naye
mmoja wa wanufaika wa elimu hiyo, daktari Bayoum Awadh,kutoka kampuni ya
Emergent Africa, aliipongeza benki ya TIB kwa kutoa mafunzo hayo kwani yatazidi
kuwaongezea elimu na uzoefu zaidi wa kuendesha biashara zao.
‘Naishukuru
sana benki ya TIB kwa kuendesha mafunzo haya, na nawaomba wajasiriamali
wenzangu wajitokeze kwa wingi kujipatia elimu hii kwani itawasaidia sana
kuendesha biashara zao kwa faida’ alisema daktari Bayoum Awadh.
No comments:
Post a Comment