Habari za Punde

Mradi wa Gewe - Tamwa wamalizika Disemba mwaka huu

 BIKOMBO Madina Hamad wa shehia ya Mjini Ole wilaya Chakechake, ambae amefanikiwa kubakia ndani ya nyumba aliokuwa ameolewa na kuachwa na watoto nane, baada ya kusaidiwa na mradi wa GEWE-TAMWA, ambapo kwa sasa ameanzisha kilimo cha mboga mboga na kujikimu walau kwa chakula, huku akiwa pia kwenye mpango wa kunusuru kaya masini kupitia TASAF III, wakati akizungumza na mwandishi wa habari Haji Nassor, (Picha na Fatma Hamad, Pemba).
 WARATIBU wa wanawake na watoto pamoja na wasaidizi wao wa shehia za Kinyikani, Kiungoni, Mjini ole, Kangagani, Mchanga mdogo na Shengejuu wakiwa katika picha ya pamoja, baada ya kumalizika kwa mradi wa GEWE –TAMWA  ndani ya shehia zao, halfa hiyo ilifanyika Tibirinzi Chakechake, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MRATIBU wa wanawake na watoto shehia ya Mjini Ole, Khadin Nenock Maziku, akizungumza na mwandishi wa habari wa shirika la magazeti ya serikali Zanzibar ofisi ya Pemba Haji Nassor, juu mafanikio ya mradi wa GEWE -TAMWA, ambao unamalizika mwezi Disemba mwaka huu (Picha na Fatma Hamad, Pemba).
 SHEHA wa shehia ya Mchanga mdogo Assa Makame Said, akitoa ufafanuzi wa namna ya kupambana na matendo ya udhalilishaji, kwenye hafla ya kufungwa kwa mradi wa GEWE-TAMWA iliofanyika Kiuyu Kigongoni wilaya ya Wete Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WARATIBU wa wanawake na watoto pamoja na masheha wa shehia sita za wilaya ya Wete, zilizokuwemo ndani ya mradi wa GEWE, wakiwa kwenye hafla ya kufungwa kwa mradi huo, iliofanyika Kiuyu Kigongoni wilaya ya Wete Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba). 

 SHEHA wa shehia Kiungoni wilaya ya Wete Pemba, Omar Khamis Othman, akizungumza kwenye hafla ya kufungwa mradi wa GEWE, uliokuwa ukiendeshwa na TAMWA, hafla hiyo ilifanyika Kiuyu Kigongoni wilayani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
SHEHA wa shehia Shengejuu wilaya ya Wete Pemba Omar Kombo, akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kufungwa mradi wa GEWE uliokuwa ukiendeshwa na TAMWA kwenye shehia sita za wilaya hiyo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.