Mwakilishi wa Tanzania  katika Umoja wa Mataifa  Balozi Tuvako  Manongi akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa  Ripoti ya  utendaji  kazi wa IRMCT ambapo  alimshukuru kwa namna ya pekee Msajili wa  IRMCT Bw. John Hopkins kwa uongozi wake na  ushirikiano  ambao ameonyesha katika ujenzi wa majengo mapya huko Lakilaki  lakini pia  katika kusimamia  kipindi cha mpito na makabidhiano kutoka  ICTR kwenda  IRMCT.
Rais wa IRMCT, Bw. Theodor Meron akiwasilisha mbele ya  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, hapo  siku ya jumatano, Ripoti ya  utendaji kazi wa  Matawi ya  Mahakama za Kimataifa za  Kesi za Masalia zinachokua nafasi ya  iliyokuwa  Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya  Rwanda ( ICTR) na  Mauaji ya halaiki yaliyotokea  katika iliyokuwa  Yugoslavia ya zamani ( ICTY. Bw. Meron  alitumia pia fursa hiyo  kuishukuru  Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa hali na  mali  katika  ujenzi wa majengo  yanayochokua nafasi ya  ICTR majengo hayo  yamejengwa katika eneo  la Lakilaki Mkoani Arusha.
Na 
Mwandishi Maalum, New York
Umoja wa Mataifa   kwa 
mara nyingine tena, umeishukuru Serikali ya  Tanzania kwa kusaidia kwa hali  na mali ujenzi na hatimaye kuelekea  ukamilishwaji 
wa Majengo  mapya ambayo
yatatumika kwa shughuli za iliyokuwa 
Mahakama ya Kimataifa   ya  Mauaji ya Kimbari  ya Rwanda ( ICTR) ambayo ilihitimisha majukumu
yake   mwaka jana.
Shukrani hizo zimetolewa siku ya  jumatano  na 
Bw.Theodor  Meron,  ambaye ni Rais wa  Mahakama 
za  Kimataifa za Kesi za Masalia
na Utunzaji wa kumbukumbu na  nyaraka
zote muhimu za zilizokuwa   Mahakama
za  Kimataifa zilizoshughulikia mauaji ya
halaiki  yaliyotokea  Rwanda na 
 Yugoslavia ya zamani ( IRMCT).
 Bw. Theodor Meron alikuwa akiwasilisha  Ripoti yake ya Nne kuhusu IRMCT mbele ya  Baraza Kuu la 
Umoja wa Mataifa . Ripoti ambayo imeanisha maendeleo ya kipindi cha
mpito  kutoka ICTR na ICTY kwenda IRMCT kazi
ambayo amesema  inakwenda vizuri ingawa
kumekuwapo na changamoto  kadhaa.
“Wakati  ninapowasilisha  ripoti 
hii, nichukue fursa hii  kutoa
shukrani zangu  za dhati kabisa kwa
mchango mkubwa na ushirikiano  ambao  tumeupata kutoka  serikali ya 
Tanzania, takribani wiki  tatu
zijazo majengo hayo yatazinduliwa rasmi baada ya kuwa yamekamilika”. Akasema
Bw. Meroe
Baadhi ya  changamoto hizo kwa upande wa iliyokuwa  ICTR 
ni  pamoja na  kutokamatwa hadi sasa kwa watuhumiwa  watatu 
ambao inaelezwa wapo  mafichoni. 
Ni pili ni  mahali pa kuwapeleka watu ambao ama wamekwisha
maliza kutumikia vifungo vyao  na kuachiwa
huru. Watu hao wamekosa nchi ya 
kuwapokea na  hadi sasa bado
wanaendelea kuishi  nchini  Tanzania.
Na kwa sababu hiyo, Rais wa  IRMCT ametoa wito kwa  Jumuiya ya Kimataifa kutoa ushirikiano wa
kuwachukua watu hao ambao  hawana  mahali pa kwenda na  kwa wale walioko mafichoni nchi ambazo
wamejificha watoe ushirikiano  kwa
kuwafichua  na kuwakamata ili hatimaye
sheria iweze kuchukua mkondo wake
Kwa 
upande wake,  Tanzania  kupitia Mwakilishi wake katika Umoja wa
Mataifa,  Balozi Tuvako Manongi,
amesema  Tanzania  inakaribisha kuhitimishwa kwa ujenzi kwa  ujenzi wa makazo mapya ya iliyokuwa  ICTR katika eneo la Lakilaki ndani ya wakati
na kwa bajeti iliyopangwa.
“Kwa namna ya  pekee tunampongeza Msajili wa  Mahakama, Bw. John Hopkins kwa uongozi wake
na ushirikiano wake ambao  umewezesha
kukamilisha hatua hii muhimu sana”. Akasisiza 
Balozi.
Aidha 
kukamilika kwa majengo hayo 
na  ambayo  yapo katika ardhi ya  Tanzania ni heshima na  fahari kubwa na ya kipekee  kwa Tanzania 
na  wananchi wake    kutokana na 
jukumu kubwa iliyobeba ya kuwa mwenyeji 
wa  Mahakama ya Kimataifa ya mauaji
 ya Kimbari ya  Rwanda 
kwa niaba ya  Jumuiya ya
Kimataifa. 
Balozi Manongi pia amepongeza
uratibu  uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa
kupitia Ofisi ya Mshauri wa  Sheria,
Ofisi  ya  Msajili na 
the  Hegue ya kuhakikisha kwamba,
pamekuwapo na utaratibu mzuri  wa
kurithishana kutoka  ICTR kwenda IRMCT.
Na kwamba kazi hiyo haikuwa nyepesi.
Akizungumzia kuhusu kazi za IRMCT,
Balozi  amesema,  Tanzania 
ingependa  kuona  Taasisi za 
Kitaifa  zinawezeshwa  ili ziweze kushughulikia  kwa 
ukamilifu, haki na usawa  na  kwa 
kuzingatia  sheria za  kimataifa kesi zinazopelekwa kwenye  Taasisi hizo za kitaifa.
Aidha akasema uzoefu ambao
umepatikana  kutokana na  kazi kubwa  
iliyofanywa na  ICTR pamoja na ile
ya  ICTY 
ni vema ukatumika  kama mfano
katika   Mahakama  nyingine za 
Kimataifa.
Kwa upande wa mashahidi, Tanzania
imesisita  umuhimu wa mashahidi kulindwa
na kuhakikishiwa usalama wao dhidi ya 
vitisho mara baada ya kutoa ushahidi.
Kuhusu  watu walioachiwa huru baada ya
kukamilisha  vifungo  vyao na bado wapo nchini Tanzania. Tanzania
imeungana na  wazungumzaji wengine katika
mkutano huo wa kutaka pawepo na 
majadiliano ya kina ya kuangalia namna 
gani ya  kuwasaidia watu hao.
Vile Tanzania imetoa wito kwa  nchi zile ambazo  zinahisiwa 
kwamba zinawahifadhi  watuhumiwa  watatu ambao wapo mafichoni na wanatakiwa
kufikishwa katika vyombo  vya sheria
kutoa ushirikiano ili  hatimaye haki
itendeke.
Watuhumiwa ambao wametajwa kuwa
walihusika kwa  namna  moja ama nyingine  katika mauaji ya  Kimbari nchini Rwanda na wapo  mafichoni hadi sasa ni Augustin Bizimana,
Felicien Kabuga na Proitas Mpiranya. 
Kwa 
mujibu wa  Ripoti  iliyowasilishwa mbele ya  Baraza Kuu la 
Umoja wa Mataifa, watuhumiwa
hao watakapopatikana  kesi zao  zitafanyika katika  Mahakama hiyo 
mpya  nchini Tanzania. 
Uamuzi kwa kuwa na  matawi 
 ya   IRMCT 
huko  Arusha na the  Hague, Uholanzi unatokana na   maamuzi ya 
Baraza la Usalama la  Umoja wa
Mataifa  kupitia azimio nambari 1966
la  mwaka 
2010.
Kupitia  Azimio hilo 
Baraza la  Usalama  liliamua   kwamba,
baada ya kumalizika rasmi kwa   ICTR (
2015) na  ICTY ( 2017) Tanzania ambayo
ndiyo ilikuwa mwenyeji wa  ICTR itapewa
jukumuu la  kuhifadhi kumbukumbu na
nyaraka zote muhimu za iliyokuwa ICTR ikiwa ni pamoja na kumalizia  kesi zitakazokuwa zimebaki. Huku  the Hague ikiwa na dhamana hiyo hiyo kwa kazi
zilizokuwa za  iliyokuwa  ICTY.
Mahakama za Kimataifa  za Rwanda na  Yugoslavia ambazo zimefanya kazi kubwa ya kuwafikisha mbele ya sheria
watuhumiwa karibu  wote waliohusika
na  matukio ya  kutisha ya ukiukwaji wa haki za binadamu
ziliazishwa mwaka  1990  na 
Umoja wa Mataifa.

No comments:
Post a Comment