Mwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa Ripoti ya utendaji kazi wa IRMCT ambapo alimshukuru kwa namna ya pekee Msajili wa IRMCT Bw. John Hopkins kwa uongozi wake na ushirikiano ambao ameonyesha katika ujenzi wa majengo mapya huko Lakilaki lakini pia katika kusimamia kipindi cha mpito na makabidhiano kutoka ICTR kwenda IRMCT.
Rais wa IRMCT, Bw. Theodor Meron akiwasilisha mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, hapo siku ya jumatano, Ripoti ya utendaji kazi wa Matawi ya Mahakama za Kimataifa za Kesi za Masalia zinachokua nafasi ya iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) na Mauaji ya halaiki yaliyotokea katika iliyokuwa Yugoslavia ya zamani ( ICTY. Bw. Meron alitumia pia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa hali na mali katika ujenzi wa majengo yanayochokua nafasi ya ICTR majengo hayo yamejengwa katika eneo la Lakilaki Mkoani Arusha.
Na
Mwandishi Maalum, New York
Umoja wa Mataifa kwa
mara nyingine tena, umeishukuru Serikali ya Tanzania kwa kusaidia kwa hali na mali ujenzi na hatimaye kuelekea ukamilishwaji
wa Majengo mapya ambayo
yatatumika kwa shughuli za iliyokuwa
Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) ambayo ilihitimisha majukumu
yake mwaka jana.
Shukrani hizo zimetolewa siku ya jumatano na
Bw.Theodor Meron, ambaye ni Rais wa Mahakama
za Kimataifa za Kesi za Masalia
na Utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka
zote muhimu za zilizokuwa Mahakama
za Kimataifa zilizoshughulikia mauaji ya
halaiki yaliyotokea Rwanda na
Yugoslavia ya zamani ( IRMCT).
Bw. Theodor Meron alikuwa akiwasilisha Ripoti yake ya Nne kuhusu IRMCT mbele ya Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa . Ripoti ambayo imeanisha maendeleo ya kipindi cha
mpito kutoka ICTR na ICTY kwenda IRMCT kazi
ambayo amesema inakwenda vizuri ingawa
kumekuwapo na changamoto kadhaa.
“Wakati ninapowasilisha ripoti
hii, nichukue fursa hii kutoa
shukrani zangu za dhati kabisa kwa
mchango mkubwa na ushirikiano ambao tumeupata kutoka serikali ya
Tanzania, takribani wiki tatu
zijazo majengo hayo yatazinduliwa rasmi baada ya kuwa yamekamilika”. Akasema
Bw. Meroe
Baadhi ya changamoto hizo kwa upande wa iliyokuwa ICTR
ni pamoja na kutokamatwa hadi sasa kwa watuhumiwa watatu
ambao inaelezwa wapo mafichoni.
Ni pili ni mahali pa kuwapeleka watu ambao ama wamekwisha
maliza kutumikia vifungo vyao na kuachiwa
huru. Watu hao wamekosa nchi ya
kuwapokea na hadi sasa bado
wanaendelea kuishi nchini Tanzania.
Na kwa sababu hiyo, Rais wa IRMCT ametoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kutoa ushirikiano wa
kuwachukua watu hao ambao hawana mahali pa kwenda na kwa wale walioko mafichoni nchi ambazo
wamejificha watoe ushirikiano kwa
kuwafichua na kuwakamata ili hatimaye
sheria iweze kuchukua mkondo wake
Kwa
upande wake, Tanzania kupitia Mwakilishi wake katika Umoja wa
Mataifa, Balozi Tuvako Manongi,
amesema Tanzania inakaribisha kuhitimishwa kwa ujenzi kwa ujenzi wa makazo mapya ya iliyokuwa ICTR katika eneo la Lakilaki ndani ya wakati
na kwa bajeti iliyopangwa.
“Kwa namna ya pekee tunampongeza Msajili wa Mahakama, Bw. John Hopkins kwa uongozi wake
na ushirikiano wake ambao umewezesha
kukamilisha hatua hii muhimu sana”. Akasisiza
Balozi.
Aidha
kukamilika kwa majengo hayo
na ambayo yapo katika ardhi ya Tanzania ni heshima na fahari kubwa na ya kipekee kwa Tanzania
na wananchi wake kutokana na
jukumu kubwa iliyobeba ya kuwa mwenyeji
wa Mahakama ya Kimataifa ya mauaji
ya Kimbari ya Rwanda
kwa niaba ya Jumuiya ya
Kimataifa.
Balozi Manongi pia amepongeza
uratibu uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa
kupitia Ofisi ya Mshauri wa Sheria,
Ofisi ya Msajili na
the Hegue ya kuhakikisha kwamba,
pamekuwapo na utaratibu mzuri wa
kurithishana kutoka ICTR kwenda IRMCT.
Na kwamba kazi hiyo haikuwa nyepesi.
Akizungumzia kuhusu kazi za IRMCT,
Balozi amesema, Tanzania
ingependa kuona Taasisi za
Kitaifa zinawezeshwa ili ziweze kushughulikia kwa
ukamilifu, haki na usawa na kwa
kuzingatia sheria za kimataifa kesi zinazopelekwa kwenye Taasisi hizo za kitaifa.
Aidha akasema uzoefu ambao
umepatikana kutokana na kazi kubwa
iliyofanywa na ICTR pamoja na ile
ya ICTY
ni vema ukatumika kama mfano
katika Mahakama nyingine za
Kimataifa.
Kwa upande wa mashahidi, Tanzania
imesisita umuhimu wa mashahidi kulindwa
na kuhakikishiwa usalama wao dhidi ya
vitisho mara baada ya kutoa ushahidi.
Kuhusu watu walioachiwa huru baada ya
kukamilisha vifungo vyao na bado wapo nchini Tanzania. Tanzania
imeungana na wazungumzaji wengine katika
mkutano huo wa kutaka pawepo na
majadiliano ya kina ya kuangalia namna
gani ya kuwasaidia watu hao.
Vile Tanzania imetoa wito kwa nchi zile ambazo zinahisiwa
kwamba zinawahifadhi watuhumiwa watatu ambao wapo mafichoni na wanatakiwa
kufikishwa katika vyombo vya sheria
kutoa ushirikiano ili hatimaye haki
itendeke.
Watuhumiwa ambao wametajwa kuwa
walihusika kwa namna moja ama nyingine katika mauaji ya Kimbari nchini Rwanda na wapo mafichoni hadi sasa ni Augustin Bizimana,
Felicien Kabuga na Proitas Mpiranya.
Kwa
mujibu wa Ripoti iliyowasilishwa mbele ya Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa, watuhumiwa
hao watakapopatikana kesi zao zitafanyika katika Mahakama hiyo
mpya nchini Tanzania.
Uamuzi kwa kuwa na matawi
ya IRMCT
huko Arusha na the Hague, Uholanzi unatokana na maamuzi ya
Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa kupitia azimio nambari 1966
la mwaka
2010.
Kupitia Azimio hilo
Baraza la Usalama liliamua kwamba,
baada ya kumalizika rasmi kwa ICTR (
2015) na ICTY ( 2017) Tanzania ambayo
ndiyo ilikuwa mwenyeji wa ICTR itapewa
jukumuu la kuhifadhi kumbukumbu na
nyaraka zote muhimu za iliyokuwa ICTR ikiwa ni pamoja na kumalizia kesi zitakazokuwa zimebaki. Huku the Hague ikiwa na dhamana hiyo hiyo kwa kazi
zilizokuwa za iliyokuwa ICTY.
Mahakama za Kimataifa za Rwanda na Yugoslavia ambazo zimefanya kazi kubwa ya kuwafikisha mbele ya sheria
watuhumiwa karibu wote waliohusika
na matukio ya kutisha ya ukiukwaji wa haki za binadamu
ziliazishwa mwaka 1990 na
Umoja wa Mataifa.
No comments:
Post a Comment