Na
Abdi Shamnah
SERIKALI
ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema itaendelea kuchukua hatua kuhakikisha maeneo
yote ya Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia (Karume Institute of Science
Technology - KIST) yanalindwa, ili kuiwezesha kufanikisha vyema malengo yake.
Imesema
pia inalengo kuongeza bajeti ya taasisi
hiyo ili kuimarisha miundo mbinu mbali mbali iliopo, ikiwemo majengo ya
wanafunzi.
Kauli
hiyo imetolewa an Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.
Ali Mohammed Shein katika viwanja vya KIST, katika kilele cha maadhimisho ya
miaka 50, tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo
1966.
Akizungumza
kwa niaba ya Dk. Shein, Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, Salama
Aboud Talib alisema tayari Wizara yake kwa kushirikiana an Wizara ya Elimu
imelipatia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa Hati miliki ya taasisi hiyo,
ilioyokosekana kwa kipindi chote hicho.
‘‘Rais
aliagiza Wizara yangu tukae pamoja na wizara ya Elimu kulipatia ufuimbuzi
tatizo hili, tayari tumeshakaa na tumeshakamilisha taaratibu zote, tuna
matarajio itapatikana mapema mwezi ujao’’, alisema.
Aidha
alisema hatua ya Rais Shein kutia saini sheria ya mafuta na gesi, namba 6 ya
2009 , ina mnasaba mkubwa na uimarishaji wa Taasisi hiyo kwa kuzingatia
mahitaji makubwa ya serikali katika upatikanaji wa wataalamu wa ndani katika
usimamizi na uendeshaji wa nishati.
Alitoa
rai kwa uongozi wa Taasisi hiyo kujipanga na kufanikisha azma iliyoweka ya
kuanzisha kozi ya stashahada kwa ajili ya fani ya mafuta na gesi asilia,
sambamba na kozi ya uhandisi wa ndege.
‘‘Hii nayo itakwenda sambamba na juhudi zinazofanywa na Serikali za kuimarisha huduma za uwanja wake wa Ndege
wa Abeid Amani Karume’’, alisema.
Katika
hatua nyengine Waziri Salama alitoa wioi kwa wanafunzi kote nchini kujikita na
kupenda kusoma masomo ya Sayansi, kwa kigezo kuwa kuna mahitaji makubwa katika
fani mbali mbali, ikiwemo ile ya ufundi.
Aliupongeza
uongozi wa tyaasisi hiyo kwa kufikia malengo ya kuanzishwa kwake, mara tu baada
ya Mapinduzi ya 1964.
Nae,
Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Mmanga Mjengo Mjawiri aliushauri
uongozi wa KIST kuanzisha masomo ya fani ya Industrial Engineering, kwa kigezo
kuwa Taifa linalenga kufanya mapinduzi makubwa kuelekea uanzishaji wa viwanda.
Mapema,
akisoma risala ya Wahitimu wastaafu, mwanazuoni Talha Masoud ,alisema pamoja na
taasisi hiyo kupata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 50, bado wahitimu
wake wanakabiliwa na changamoto kadhaa, ikiwemo ukosefu wa ajira, hususan
katika taasisi za serikali, huku taasisi binafsi nazo zikielezwa kuajiri
wahitimu wachache.
Aliiomba
Serikali kuweka kipaumbele kwa makampuni ya ujenzi ya wazalendo katika miradi
mbali mbali, ikiwa njia mojawapo ya kutoa fursa za ajira kwa vijana.
Aidha
alikososa utaratibu wa kutokuwepo uwiano wa kimaslahi kati ya watendaji wa
taasisi hiyo na taasisi nyingine, ikiwemo kada za udaktari na wanasheria.
Aliiomba
Serikali iondokane na upendeleo, na kuzichukulia kada hizo kwa mizania iliyo
sawa, kwa kigezo kuwa zote ni muhimu katika mustakbali wa maendeleo ya Taifa.
Aliongeza
kwa kusema kuwa pale chanagamoto hiyo itakapopatiwa ufumbuzi, ni wazi kuwa
wanafunzi wengi watapenda kusoma masomo ya hayo ya ufundi.
Pamoja
na kutembelea maonyesho mbali mbali katika sherehe hizo, Waziri Salama alipata
fursa ya kukabidhi vyeti kwa wakufunzi na wahitimu waliodumu na utumishi wa
kipindi kirefu ndani ya taasisi hiyo
tangu ilipoanzishwa 1966.
No comments:
Post a Comment